Na Victor Bariety – Geita
Wakati dirisha la kuchukua na kurejesha fomu ndani ya CCM kwa ajili ya kuwania Ubunge wa Geita Mjini likiwa limefunguliwa rasmi, hali ya kisiasa imeingia kwenye hatua ya pili—vita ya vipaumbele. Sio tena nani ana mashabiki wengi au konvoy kubwa, bali nani anajua anachotaka kufanya kwa wananchi wa Geita.
Kwa mujibu wa Katibu wa CCM Wilaya ya Geita, Bw. Michael Msuya, jumla ya watia nia 18 wamejitokeza. Lakini kwa jicho la wachambuzi wa siasa na mitazamo ya wananchi mitandaoni, mapambano ya kweli yako kati ya waliowahi kushika nyadhifa, walioleta mabadiliko, na wenye ndoto kubwa zinazoweza kupimika.
1. KANYASU: VIPAUMBELE VYA MADINI NA MAZINGIRA
Mbunge anayemaliza muda wake, Mh. Constantine Kanyasu, amejijengea jina kupitia vipaumbele vyake vilivyolenga wachimbaji, sekta ya madini, mazingira na sera za kitaifa.
Vipaumbele vyake vilivyowahi
kutekelezwa:
Kuanzisha maabara ya mionzi kwa ajili
ya kupima madini Geita.
Kutetea fidia ya wananchi waliopata
madhara ya mitetemo kutoka migodini.
Kuunga mkono kiwanda cha kusafisha
dhahabu (GGR) – kilichozalisha ajira zaidi ya 100.
Kupigia debe upandaji wa miti baada
ya uchimbaji – sera ya madini endelevu.
Kama ataendelea, Kanyasu anasema kipaumbele chake ni:
“Kuboresha mazingira ya wachimbaji
wadogo, kuunganisha sekta ya madini na vijana wanaomaliza vyuo kwa mafunzo ya
kiufundi.”
2. MANJALE MAGAMBO: VIPAUMBELE VYA VIJANA NA MAWASILIANO MAPYA
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Geita, Manjale Magambo, anaungwa mkono na vijana wengi kwa sababu ya historia ya kuwatetea na kuwawezesha.
3. CHACHA WAMBURA: VIPAUMBELE VYA ELIMU NA UWEKEZAJI
Mmiliki wa shule za Waja na msomi mwenye mtazamo wa kitaasisi, Chacha Wambura, anaamini elimu ndio msingi wa maendeleo ya mji.
Vipaumbele vyake vinavyopigiwa debe na wafuasi:
Kuweka msukumo mkubwa kwenye elimu bora ya msingi hadi chuo.
Kuanzisha mfuko wa mikopo kwa wanafunzi wanaotoka familia duni.
Kujenga vituo vya ubunifu (innovation hubs) kwa vijana wa Geita.
Ananukuliwa akisema:
“Tusipojenga watu, hatuwezi kujenga mji—elimu ni dhamira yangu ya msingi.”
4. INJINIA ROBERT GABRIEL: VIPAUMBELE
VYA MIUNDOMBINU NA UTENDAJI
TATHMINI YA KITAALUMA: VITA YA VIPAUMBELE SI YA KUSUKUMWA NA HISIA
Katika uchaguzi huu, Geita inakabiliwa na uchaguzi mgumu lakini muhimu sana. Si uchaguzi wa nani ana kipaza sauti kizuri au bango la kisasa, bali nani ana dira, na nani anaweza kuitafsiri dira ya taifa kwa muktadha wa Geita.
HITIMISHO: SIASA NI VITA YA MAWAZO – SI KELELE ZA MITANDAONI
Kama kweli wananchi wa Geita Mjini wanataka mabadiliko chanya, basi uchaguzi huu usiwe wa ushabiki wa WhatsApp wala kelele za wapambe. Badala yake, uwe uchaguzi wa hoja, mikakati na maono yatakayomkomboa kijana wa Geita, mama wa soko, mzee wa kijiji na mfanyabiashara wa kati.
Katika vita ya vipaumbele—tusichague jina, tushikilie dira.
Victor Bariety
Mwandishi wa Habari, Mchambuzi wa
Siasa – Geita
MWISHO
0 Comments