Na Gharos Riwa, Geita
Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Geita wameagizwa kuanza michakato ya upatikanaji wa madampo ya kisasa ili usafi unapofanyika taka ziweze kuhifadhiwa na kuchakatwa bila kuchafua mazingira.
Agizo hilo limetolewa na Kaimu katibu tawala mkoa Herman Matemu, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Geita Bi Rosemary Senyamule kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani yaliyofanyika kimkoa katika viunga vya shule ya sekondari ya Waschana Nyankumbu leo juni 5, 2022
Mipango kama hiyo amesema inabidi tangu Halmashauri zinapoandaa bajeti zao wahakikishe kwamba zinakuwepo ili hayo madampo ya kisasa yaweze kujengwa katika kila Halmashauri. Pia amesema ni wajibu wa kila mwananchi kuanzia ngazi ya familia kujitafakari ni kwa kiasi gani maamuzi anayoyafanya yanaweza kutunza mazingira na kwa ngazi ya taasisi ni kwa kiasi gani waajiri na wenye mamlaka wanatambua umuhimu wa mazingira na kuhamasisha upandaji miti.
Katika taarifa ya utekelezaji
wa uhifadhi wa mazingira iliyoseomwa na kaimu katibu tawala mkoa Geita Charles
Chacha, imebainika kwamba hali ya
mazingira katika machimbo hutofautiana ambapo wachimbaji wakubwa na wakati ni
salama kwa shughuli za hifadhi za mazingira huku wachimbaji wadogo ndiyo wenye changamoto
katika uhifadhi wa mazingira.
Taarifa hiyo imebainisha
kwamba mkoa wa Geita ina misitu hekta laki mbili mia tano hamsini na nane nukta
tatu (200,558.3) kati ya maeneo hayo sita yanamilikiwa na wakala wa misitu Tanzania-
TFS, maeneo mengine sita yanamilikiwa na mamlaka za Serikali za mitaa.
“Pamoja na kuwa na misitu
ya asili mkoa wa Geita umepanda miti milioni tatu, mia nane ishirini na tano
,mia tatu kumi na tatu kwa mwaka wa 2021/2022” alisoma Charles chacha.
Taarifa hiyo imeendelea kubainisha
kwamba Malengo ya upandaji miti ilikuwa ni kufikia milioni tisa lakini, miti
iliyopandwa ni milioni tatu, mia nane ishirini na tano ,mia tatu kumi na tatu
na miti iliyopona ni milioni tatu themanini elfu mia saba hamsini na tatu huku miti hiyo
iliyopandwa ni sawa na asilimia 42.5% .
Charles Chacha amesema
changamoto kubwa iliyokwamisha kufikia malengo ni upungufu wa miche ya miti,
hivyo serikali imeweka mikakati ya kuyafikia malengo hayo kwa kutumia taasisi
zake 66 za elimu na mpaka sasa miche milioni
mbili imeshapatikana.
| Wanafunzi na wananchi walioshiriki kwenye maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani Mkoani Geita Juni 6,2022 |
Vile vile amesema Pamoja na
faida kubwa inayopatikana kutokana na shughuli za uchimbaji wa madini katika
mkoa wa Geita zipo changamoto za kimazingira zinazo sababishwa na wachimbaji wadogo
kwenye maeneo ya vyanzo vya maji na hifadhi za misiti akitolea mfano katika maeneo
ya Mgusu mjini Geita, Nyarugusu na
Rwamgasa katika Halmashauri ya wilaya ya Geita.
Hata hivyo amesema mkoa
umeshatoa maelekezo kwa wachimbaji wadogo wote wanaofanya shughuli za madini kuwa
na mpango wa matumizi bora ya mazingira pamoja na mpango wa hifadhi za
mazingira katika sehemu zao za kazi ili kuhifadhi mazingira na kutofanya
shughuli za uchimbaji maeneo ya vyanzo vya maji kwa umbali wa mita 60.
Moja ya chanzo cha maji kilichoathiriwa na shughuli za uchimbaji wa madini
ni pamoja na mabubi liliko Mgusu na machinjioni Wilaya ya Geita.
Katika kuzuia madhara
yasiendelee kutokea mkoa kwa kushirikiana na ofisi ya mazingira pamoja na wakala
wa misitu kanda, wanafanya juhudi katika kutoa elimu,ushauri na kusimamia
sheria ya mazingira namba 20 ya mwaka 2004, na ile namba 14 ya misitu ya mwaka
2002 pamoja na sheria ndogo zote za Halmashauri.
Maadhimisho hayo
yamefanyika kitaifa mkoani Dodoma na Mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu Kasim
Majaliwa na yameongozwa na kaulimbiu “Tanzania
ni moja tu, Tunza Mazingira” .
mwisho.
0 Comments