TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

MSAJILI WA HAZINA AYATAKA MASHIRIKA YA UMMA KUWA WASIKIVU KWA MAONI YANAYO TOLEWA KUHUSU UWEKEZAJI NCHINI.

 Na Urban Epimark,  DAR ES SALAAM 

Msajili wa Hazina Bw Neemia Mchechu ameya  taadharisha mashirika ya umma nchini kuwajibika ipasavyo kwa kumwelewa vizuri Rais Dkt Samia Suluhu Hassan anavyo taka kuhusu uwekezaji nchini na kuwataka wawe wasikivu wazuri katika kupokea maoni ya wadau ili kuboresha na kuvutia uwekezaji nchini. 

Msajili wa Hazina Bw Neemia Mchechu ambae alikuwa Mgeni Rasmi katika mkutano wa kwanza wa wadau wa usafirishaji mizigo kwa njia ya Anga nchini ulio andaliwa na ATCL akiongea na washiriki katika mkutano huo. Pembeni yake kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa ATCL Mhandisi Ladislaus Matindi March 20, 2023.

Bw Mchechu ameyasema hayo kwenye mkutano wa wadau wa usafirishaji mizigo kwa njia ya anga ulio andaliwa na Shirika la Ndege nchini ATCL ulifanyika jijini Dar es Salaam March 20, 2023.

"Ofisi ya Msajili wa Hazina ndio inayo simamia mashirika yote nchini hivyo ni vizuri mashirika ya umma yakamwelewa vizuri Rais Dkt Samia kuhusu uwekezaji unao utaka nchini hususani kwa kusikiliza vizuri maoni na ushauri unao tolewa na wadau wa uwekezaji ili boresha mazingira ya kuvutia uwekezaji zaidi kutoka nje" alieleza Msajili.

Baadhi ya washiriki wa mkutano wa wadau wa usafirishaji mizigo kwa njia ya Anga hapa nchini ulioandaliwa na ATCL wakiendelea mkutano huo katika ukumbi wa Golden Jubilee jijini Dar es Salaam March 20, 2023.

Bw Mchechu ambae ndie alikuwa Mgeni Rasmi katika mkutano huo uliojumuisha wadau mbalimbali wa sekta ya usafirishaji mizogo kwa njia ya anga ulio andaliwa na ATCL alisema, ili uwekezaji ufanye vizuri zaidi nchini, sekta ya umma inabidi kwenda na kasi ya Sekta Binafsi ili mambo yaende sawa.

Amezishauri taasisi mbalimbali za umma zinazo wajibika kwenye mlolongo wa uwekezaji pamoja na upande wa kodi kuwajibika zaidi na kuwa radhi muda wote kusikiliza maoni ya wadau ili kuondoa baadhi ya vikwazo katika kutanua uwekezaji zaidi nchini.

Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa kampuni ya usafirishaji mizigo kwa njia ya Anga ya Swissport Tanzania Bw Mrisho Yassin (kulia mwenye suti nyeusi) akiwa kwenye mazungumzo na Afisa Mtendaji Mkuu wa GS1-TANZANIA Bi Fatuma Kange (kushoto) wakati wa mapumziko wa mkutano huo jij8ni Dar es Salaam March 20, 2023

Nae Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya usafirishaji mizigo kwa njia ya Anga ya Swissport Tanzania Bw Mrisho Yassin ameishauri Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) kuwa "flexible" katika kusimamia sheria za kodi husani kwenye mpango wa ushirikiano wa kiubia kati ya sekta ya Umma na Binafsi nchini yaani "Public Private Partinaship-PPP" 

Bw Yassin aliilalamikia TRA inavyoibana Swissport Tanzania katika kufanya uwekezaji zaidi kwenye miundo mbinu inayo husisha umiliki wa ardhi na kusema, Swissport inashindwa kuwekeza zaidi nchini kutokana na muundo wa sheria hiyo ya "Public Private Partinaship" ambapo wao hawamiliki ardhi hapa nchini.

Msajili wa Hazina Bw Neemia Mchechu (kushoto) akikabidhiwa zawadi maalumu na Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa ATCL Mhandisi Ladislaus Matindi (kulia) kwenye mkutano huo ulio andaliwa na ATCL jijini Dar es Salaam March 20, 2023. Msajili wa Hazina alikuwa Mgeni Rasmi katika mkutano huo.

Msajili wa Hazina Bw Neemia Mchechu (katikati mstari wa mbele) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa ATCL na wadau wengine baada ya kumalizika mkutano huo jijini Dar es Salaam March 20, 2023.

Mwisho.

Post a Comment

0 Comments