Anna Ruhasha, Mwanza.
Mweyekiti wa jumuiya ya wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Wilayani Sengerema mkoani Mwanza Jacksoni Mazinzi ametoa kadi za CCM Elfu Moja za jumuiya ya wazazi kwaajili ya kupunguza changamoto ya uhaba wa upatikanaji wa kadi kwa wanachama wa jumuiya hiyo.
Mazinzi ametoa kadi hizo wakati akitekeleza ahaadi yake mbele ya wananchama wa jumuiya hiyo aliyoiahidi wakati akiomba kura ya za ndiyo katika uchaguzi mkuu ndani ya ccm ya kutafuta viongozi katika jumuiya hiyo.
Aidha katika uchaguzi huo ulifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita na kufanyikia katika ukumbi wa Sengerema sekondari Mazinzi alitangazwa kuwa mshindi na msimamizi wa uchaguzi Mwashamu Ismail kuwa Mazinzi alipata kura 371
Hata hivyo Mazinzi akiwashukuru wajumbe kwa kumchagua amesema kuwa katika uongozi wake katika kipindi cha miaka mitano atahakikisha anapunguza changamoto zinazozikabili jumuiya hiyo .
“nimeamua kugombea nafasi hii kwa sababu nimebaini jumuiya hii imekuwa ikikabiliwa na changamoto kama vile uelewa juu ya mambo Kadha wa kadha ya jumuiya niwaambie wanancha nitaanza kutoa semina kwenu “Mazinzi.
Ali kadhalika aliyekuwa mbunge wa jimbo la Buchosa Dk Charlse Tizeba mmoja ya wachaguliwa katika uchaguzi huo ambapo amechaguliwa kuwa mwakilishi mkutano mkuu taifa kupitia jumuiya ya wazazi pia akizungumza na wapiga kura baada ya kutangazwa kuwa mshindi amesema ataitumikia jumuiya hiyo kwa ufasaa kutokana na uzoefu alionao hasa katika kudumisha umoja kwa wanancha.
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wilayani Sengerema mkoani humo Agustine Makoye amesema kuwa uchaguzi ulifanyika ni kwamujibu wa katiba ya chama ,uku Katibu wa chama hicho wilaya Muksin Zikatimu ameongeza kuwa uchaguzi ngazi za jumuiya umeisha na kuwata viongozi waliochaguliwa kwenda kufanya kazi za chama kwa weledi.
Mwisho

0 Comments