TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

CONSOLATHA AAHIDI KUFANYA KAZI KWA WELEDI

Consolatha Charles Malunde mshindi wa kwanza Baraza wilaya kwa kuibuka na kura 365 kati ya kura zilizopigwa 552.

 ANNA RUHASHA-MWANZA 

Viongozi wa jumuiya ya wananwake  wa chama cha Mapinduzi CCM wilayani Sengerema mkaoni mwanza  Wamesema  kuwa watahakikisha wanasimamia yale yote waliyoahidi  kuyatekeleza katika uongozi wao kwa kipindi cha miaka mitano.

Hayo yamezungumzwa na baadhi ya viongozi waliochaguliwa katika uchaguzi mkuu    ndani ya chama cha mapinduzi CCM  katika jumuiya ya wanawake  wilayani Sengerema mkaoni humo.

Akizungumzia kwa niaba ya wenzake mmoja ya wagombea ambae ameibuka mshindi nafasi ya  mjumbe Halmashauri kuu wilaya  Consolatha  Malunde.

Amewashukuru wajumbe kwa kumuamini kumpa nafasi hiyo licha ya kutumikia nafasi mbali mbali katika chama hicho “nawashukuru kwa kupigiwa kura zaidi 346 na kuwa mshindi wa kwanza kati  ya wagombea 21 ambao tuliwania nafasi hii wajumbe hawa nitawalipa kwa kufanya kazi kwa weledi " amesema  Malunde.

 Aidha ameongeza kuwa  jumuiya  ya wanawake ni jumuiya yenye miradi mingi ya maendeleo kwa kushirikiana na viongozi waliochaguliwa atatoa ushirikiano  ili kuhakikisha  jumuiya inapiga hatua zaidi.

 Katibu wa UWT wilaya   Rosemary Mwakasalo amesema kuwa  uchaguzi umefanyika kwa amani na  kumalizika salama ambapo amesema kuwa jumuiya  ya wanawake imechagua kiongozi ngazi ya wilaya ,mjumbe wawakilishi ngazi ya wilaya na mkoa , wajumbe wa halmashauri kuu wilaya pamoja na  mwakilishi ngazi ya Taifa.


Mwisho

Post a Comment

0 Comments