TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

VIBOKO SIYO NJIA YA UFUNDISHAJI: DC SENGEREMA

Mkuu wa wilaya ya Sengerema Senyi Ngaga akizungumza katika uzinduzi wa miongozo ya kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji ngazi ya elimu  Msingi  na Sekondari

Na Anna  Ruhasha, Sengerema.

Walimu wa shule  za Msingi na Sekondari  Wilayani Sengerema Mkoani  Mwanza wameonywa  kutotumia viboko  kupita kiasi kama njia ya ufundishaji kwa wanafunzi  jambo ambalo linapelekea wanafunzi kuchukia masomo pamoja na kuacha shule. 

Onyo hilo limetolewa na Mkuu wa wilaya ya Sengerema Mhe Senyi Ngaga wakati akizindua miongozo ya kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji  ngazi ya Elimu Msingi na Sekondari  kwa lengo la kuboresha Elimu katika ukumbi wa mikutano wa shule ya sekondari Sengerema.

Amesema kuwa kumekuwepo na tabia ya baadhi ya walimu kuwachapa viboko wanafunzi kila siku  hali ambayo inasababisha wanafunzi kuwa watoro na kuichukia shule.

Afisa elimu shule za msingi katika halmashauri ya Wilaya ya Sengerema  Mwl. Donalti Bunonos  amesema kuwa  miongozo hiyo  itakuwa chachu  ya kuboresha ufundishaji  kwa wanafunzi na kuahidi kwenda kuitekeleza ipasavyo.

Nao baadhi ya wakuu wa shule wameahidi kwenda  kuisoma na kuielewa miongozo hiyo  ili iweze kuwasaidia kuongeza ufaulu kwa wanafunzi katika shule zao.


 Mwisho

Post a Comment

0 Comments