Na Beatus Bihigi, Geita.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara na Uwezeshaji kutoka Wizara ya Maendeleo ya Viwanda Vidogo na Vya Kati kutoka Nchini Zambia ametembelea Mabanda ya Maonyesho ya Tano ya Teknolojia ya Madini.
Mkurugenzi huyo ametembelea Mabanda yenye Vifaa vya Kisasa Kutoka Mgodi wa Geita(GGML) na migodi ya wachimbaji wa kati na wadogo na kushuhudia Vifaa hivyo vinavyofanya kazi kwenye maeneo ya migodi wakati wa uzalishaji wa madini ya dhahabu.
![]() |
| Muwakilishi wa Waziri kutoka Zambia Kennedy Mumba alievaa Shati la drafts akipata maelezo na Geofrey Meena ambaye ni Meneja Masoko na mahusiano ya umma katika banda la STAMICO leo 1 Oktoba 2022. |
Aidha,ameipongeza serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutambua umuhimu wa wachimbaji wadogo kwa kuonyesha shughuli wanazofanya kupitia maonesho hayo,ambapo ameahidi kwa mara nyingine Zambia kushiriki maonyesho hayo.
Muwakilishi wa Waziri wa viwanda biashara na Uwekezaji kutoka Zambia amepata wasaa wa kutembelea mabanda mbalimbali ya maonesho ikiwemo banda la GGML,banda la benki kuu ya Tanzania (BoT), STAMICO , GEREMA , GEWOMA, Blue Coast na banda la kliniki ya Biashara ambapo amekiri kujifunza mengi mazuri ambayo atayafikisha kwa wafanya biashara wa Zambia.
![]() |
| Mwakilishi wa kampuni ya usafishaji akielezea ambayo kampuni hiyo ya Blue Coast inavyo toa huduma kitaifa na kimataifa mbele ya Kennedy Mumba kutoka Zambia. |
![]() |
| Banda la GGML mmoja wa Maofisa wake akielezea upatikanaji wa madini ya Dhahabu kitaalam zaidi mbele ya Kennedy Mumba muwakilishi wa Waziri wa Maendeleo ya viwanda na biashara wa Zambia. |







0 Comments