![]() |
| Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) JAckson Mazinzi akikabidhi taulo za kike kwa baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Nyampulukano. |
Anna Ruhasha, Mwanza.
Katika kuadhimisha miaka 46 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM ), Jumuiya ya wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Sengerema Mkoani Mwanza imetoa msaada wa taulo za kike na madaftari kwa wanafunzi wanaoishi katika mazingira magumu katika shule ya Sekondari Nyampulukano pamoja na kupanda miti mia tano (500) katika shule hiyo.
![]() |
| Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) JAckson Mazinzi akikabidhi daftari kwa baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Nyampulukano. |
Akikabidhi vifaa hivyo kwa wanafunzi wa shule hiyo Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Sengerema Jackson Mazinzi amesema kuwa Jumuiya hiyo imetoa vifaa hivyo ili kuwasaidia wanafunzi kusoma katika mazingira rafiki, na kuwaagiza walimu wa shule hiyo kusimamia kikamilifu miti hiyo 500 ili iweze kukua.
![]() |
| Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jackson Mazinzi akiongoza zoezi la kupanda miti ili kutunza mazingira katika shule ya sekondari Nyampulukano. |
Baadhi ya Wanafunzi wa shule hiyo walio pewa misaada hiyo wameishukuru Jumuiya ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuwapatia vifaa kwa kuwa vitawasaidia kusoma katika mazingira rafiki.
Naye makamu mkuu wa shule ya Sekondari Nyampulukano Maemba Katemba ameipongeza Jumuiya hiyo kwa kupanda miti 500 katika shule hiyo na kutoa misaada hiyo kwa wanafunzi.
Awali katibu wa Jumuiya ya wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Sengerema Jamal Twalib Athuman amewashukuru viongozi wa Jumuiya hiyo kwa kujitokeza kwa wingi na kushiriki zoezi hilo la upandaji miti na utoaji wa msaada wa vifaa hivyo muhimu kwa Wanafunzi wa kike wawapo shuleni.
Mwisho.






0 Comments