TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

KASENDAMILA AWAOMBA WAGOMBEA ,WANACCM BUSANDA WAWEKE PEMBENI VINYONGO, WAJIKITE KUTAFUTA KURA ZA CCM.

Na mwandishi wetu;

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Geita, Nikolaus Kasendamila, amewataka wagombea na wanachama wa chama hicho waliokuwa wakihusishwa na mchakato wa kuwania nafasi za udiwani katika Jimbo la Busanda kuweka pembeni makovu na vinyongo vilivyotokana na kura za maoni, na kuelekeza nguvu katika kutafuta kura za ushindi kwa wagombea wa CCM.

 

Akizungumza katika kikao maalum kilichofanyika kata ya Nyarugusu, Kasendamila amesema anakiri kuwepo kwa mikwaruzano na mipashano miongoni mwa wanachama wakati wa mchakato wa ndani wa uteuzi, lakini akasisitiza kuwa sasa ni wakati wa umoja na mshikamano ili kuhakikisha chama kinashinda kwa kishindo.


 "Ninatambua kulikuwa na sintofahamu na mikwaruzano kwenye baadhi ya kata, lakini hayo yamepita. Tunachotakiwa sasa ni kuelekeza nguvu zetu kwenye kutafuta kura kwa wagombea wa CCM  madiwani, mbunge, na mgombea urais Dkt. Samia Suluhu Hassan," amesema Kasendamila.

Amesisitiza kuwa kwa kazi kubwa iliyofanywa na Rais Dkt. Samia katika awamu hii, hakuna sababu ya CCM kutoshinda kwa kishindo, na hivyo ni wajibu wa viongozi wa chama, madiwani, na wabunge kuhakikisha ushindi huo unapatikana kwa ushirikiano na umoja.

  "Kwa kazi iliyofanyika awamu hii ya Dkt. Samia, hakuna sababu ya kutoshinda kwa kishindo,Hii ni dhamana yetu sote kuhakikisha ushindi huu unapatikana na CCM tuwaeleze wananchi ilani iliyopita ilitekelezaje miradi na inayokuja inakwenda kufanya nini" Kasendamila


PICHA ZAIDI







 

Post a Comment

0 Comments