TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

Dkt. JAFARI ASHIRIKI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU 2025 MKOANI GEITA


Na Mwandishi wetu;

Mgombea ubunge wa Jimbo la Busanda kwa tiketi ya CCM, Dkt. Jafari Rajabu Seif, leo Septemba 1, 2025, ameshiriki katika mapokezi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru uliopokelewa rasmi leo Mkoani Geita.

Shughuli hiyo imefanyika katika Kijiji cha Rwezera, Halmashauri ya Wilaya ya Geita, ikiwa ni sehemu ya mapokezi ya mbio hizo zitakazodumu mkoani humo hadi Septemba 6, 2025.

Katika mbio hizo, Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kukagua, kuzindua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo inayofikia jumla ya miradi 61, yenye thamani ya takriban shilingi bilioni 164.

Dkt. Jafari amepongeza jitihada za serikali katika kusimamia maendeleo na kuahidi kushirikiana kwa karibu na wananchi wa Jimbo la Busanda katika kuhakikisha miradi hiyo inaleta tija kwa jamii.


Post a Comment

0 Comments