Na Renatus
Masuguliko-Sengerema;
Wakazi wa kata ya
Bitoto wilayani Sengerema mkoani Mwanza wamesema kuwa hatua ya aliyewahi kuwa Mbunge wa jimbo la
Sengerema William Mganga Ngeleja ya kuwajengea shule ya sekondari kwa fedha yake
imegeuka chachu ya elimu katika kata
hiyo.
Imedaiwa kuwa hatua
hiyo imewanusuru watoto wa kike kutowekwa vimada, wengine kufanywa nyumba ndogo na kuolewa kutokana
na awali kulazimika kupanga mitaani kutokana na shule kuwa mbali.
Kutokana na kuwepo
kwa hatua hiyo baadhi ya wadau wa maendeleo ikiwemo katika sekta ya elimu
wameomba kuhuishwa kwa mchakato wa awali uliokuwepo wa kutaka kumuenzi kwa shule hiyo kupewa jina lake
hatua itakayowatia moyo pia wadau wengine katika kuchangia shughuli za
kijamii za maendeleo.
Mwenyekiti
mstaafu wa serkali ya kijiji cha Bitoto Sangija Nguno aliyesimamia na kuratibu
ujenzi wa sekondari hiyo amesema jana kijijini hapo kuwa fedha iliyotumika
kujenga sekondari hiyo ni ya Ngeleja binafsi na yeye ndiye aliyekuwa mratibu na
msimamizi mkuu wa ujenzi huo ulioanza
mwaka 2017 na kukamilika na kuanza kupokea wanafunzi toka mwaka 2010.
Nguno ambaye
amekuwa mwenyekiti wa serkali ya kijiji cha Bitoto kwa zaidi ya miaka 20 anadai
kuwa huo ulikuwa ni mkakati wa Ngeleja wa kuwaondolea kero wanafunzi wanaochaguliwa
kujiunga na sekondari wa kiwemo wa kike kusafiri umbali wa kati ya kilometa 20 kwenda na kurudi.
Ili kuunga mkono
juhudi zake, Jamii ilibuni utaratibu wa kuhakikisha kila mzazi anayesaidia au
kushiriki kukatisha masomo ya mtoto
wakike kwa lengo la kumuozesha kuhakikisha anaadhibiwa na jamii na kila mwanajamii ni
mlinzi wa mtoto wakike utaratibu ambao umekuwa
chachu katika jimbo la Sengerema na kuzaa matunda yaliyokusudiwa.
“Uwekezaji
alioufanya Ngeleja kwa kujenga sekondari hiyo hautasahaulika, kwani unaendana
na maono ya Rais Samia Suluhu Hassan anayoyahubiri sasa ya kuhakikisha elimu
kwa mtoto wa kike inapewa
kipaumbele” alisema Mzee Nguno.
Kutokana na
sekondari kuwepo umbali mrefu hatua hiyo ndiyo iliyowalazimisha wanafunzi wakiwemo wakike kupanga mitaani
ambako baadhi yao walifanywa vimada, nyumba ndogo na kuolewa hivyo kukatisha
ndoto zao za masomo.
Kabla ya kujengwa
kwa sekondari hiyo ambayo awali wananchi waliomba ipewe jina la Ngeleja lakini
Ngeleja mwenyewe alikataa kuitwa kwa jina lake lakini kwa sasa wananchi wanadai
wanaomba mchakato huo wa kumuenzi kwa kuiita shule sekondari hiyo jina lake
uhuishwe upya.
Wanatetea hatua
hiyo kutokana na mchango wake huo, ambao umeonesha kuwa msaada mkubwa na chachu
ya elimu katika kata na jimbo la Sengerema kwa kupunguza umbali wa kutembea
kati ya kilometa kumi kufikia shule jirani za sekondari zikiwemo za Buyagu na Ngoma sekondari lakini
sasa wanatembea umbali wa kati ya
kilometa sufuri hadi kilometa mbili tu
kufika shule hivyo kuwatia moyo kutimiza ndoto zao.
Dotto Maguzu mmoja
wa wadau wa Elimu na maendeleo katika kata ya Bitoto anasema kuwa hatua hiyo
inastahili kupongezwa na kumuenzi kwa
wananchi wanahakikisha kila mtoto
wakike anayefaulu kujiunga na sekondari anatimiza ndoto yake kwa jamii kuweka
utaratibu wa kumbana kila mzazi kuhakikisha anawajibika kuanzia ngazi ya
familia hadi jamii.
Wanafunzi
Martha Peter anayesoma kidato cha tatu
katika sekondari ya Bitoto na Herena Musa anayesoma kidato cha kwanza katika
sekondari ya Bitoto wanasema kuwa uwepo
wa sekondari hiyo umegeuka chachu kwa
wanafunzi hasa wa kike kutimiza ndoto zao ikilinganishwa na wenzao waliowatangulia.
“Kwa sasa hakuna
mwanya tena wa kusingizia
kukwepa kufika sekondari wakati ule wenzetu waliotutangulia walikumbana
na vishawishi vingi njiani, ikiwemo kuishia kuolewa na kupewa ujauzito kutokana na kulazimika kusafiri umbali mrefu
na mara nyingine kupanga mitaani” alidai Martha
Kwa upande wake
Herema anayesoma kidato cha kwanza katika shule ya sekondari ya Bitoto anasema
kuwa kwa sasa wasichana wamehamasika kutimiza
ndoto zao bila kusahau kumshukuru
aliyetumia rasimali zake kujenga sekondari hiyo ili kumuenzi wanafunzi wa kike wamedai
watamuenzi kwa kusoma kwa bidii ili
kutimiza ndoto zao.
Awali Kabla ya
kujengwa sekondari ya Bitoto Wanafunzi
kutoka vijiji ikiwemo kata ya Bitoto
walikuwa wanalazmika kufuata sekondari katika kata jirani za Buyagu na Ngoma
umbali wa zaidi kilometa ishirini kwenda
na kurudi hatua iliyowalazimisha wanafunzi kupanga vyumba mitaani ili wawepo
karibu na shule hatua iliyochangia baadhi kukatisha masomo na utoro.
William Mganga
Ngeleja aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la sengerema kutoka mwaka 2005 hadi 2020
alipotakiwa kuzungumzia hatua ya yeye kukataa kwa sekondari hiyo kuitwa jina
lake amesema ilikuwa ni mapema mno kufanya hivyo.
Hata hivyo Ngeleja amesema hana kizuizi cha kuzuia
maamzi ya wananachi ambao ndio wadau wa maendeelao kutimiza adhima yao kwani yeye baada ya kukamilisha
ujenzi huo aliikabidhi kwa mamlaka husika na lengo lake kubwa lilikuwa
kumaliza kero ya muda mrefu iliyokuwa
ikiwakabili wanaochaguliwa kujiunga na sekondari hasa wasichana kwani wengi wao walikuwa
wanakatisha kumaliza masomo kutokana na umbali.
Mwisho.

0 Comments