TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

MGANGA MKUU WA SERIKALI PROF ABEL MAKUBI - WATUMISHI WAZEMBE SEKTA YA AFYA HAWATAVUMILIWA NCHINI

 


  Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi amewatahadhalisha watumishi wazembe na wanaotoa lugha chafu kwa  wagonjwa kuwa hawatavumiliwa kwa kuwa kwa kufanya hivyo nikukiuka sheria za utumishi. 

Ametoa kauli hiyo Desemba 03, Mwaka huu katika kikao kilichowakutanisha wadau wa Afya na Elimu Mkoani Geita katika ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere uliyopo halmashauri ya Mji wa Geita nakuwakumbusha wataalamu wa afya kuendelea kutoa elimu ya Magonjwa yasiyo ya kuambukiza kwa kuwa yamekuwa tishio hapa nchini.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita Dkt Japhet Simeo
 

Akiwa katika kikao hicho Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita Dakta Japhet Simeo amewataka watumishi wote kufanya kazi kwa kuzingatia sheria za utumishi Ili kuepuka migogoro na serikali nakumhakikishia Mganga mkuu wa serikali kuwa atahakikisha watumishi wazembe katika mkoa huo hawatavumiliwa. 

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandis Robert Gabrie

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandis Robert Gabriel ambae alikuwa Mgeni rasmi katika kikao hicho amewataka watumishi wa Afya na Elimu Mkoani Geita kutimiza majukumu yao bila kusukumwa kwakuwa uongozi siyo starehe.

Wadau wa Afya Mkoani Geita wakiwa katika kikao cha pamoja

 


 

Post a Comment

0 Comments