TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

MKUU WA WILAYA YA CHATO AFUTA LIKIZO ZOTE KWA WATUMISHI WA SERIKALI WILAYANI HUMO

 

Mkuu wa wilaya ya Chato Mhandis Charles Kabeho

Mkuu wa wilaya ya Chato Mkoani Geita Mhandis Charles Kabeho amefuta likizo zote kwa watumishi wa serikali katika wilaya hiyo, nakuwaagiza kutumia kipindi cha mwezi mmoja kufanya ukamilifu wa ujenzi wa vyoo na madarasa yaliyo katika hatua ya mwisho, kabla ya shule kufunguliwa mwaka kesho.

Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Chato Baada ya kuapishwa

Akizungumza katika uzinduzi wa baraza la madiwani wilayani humo Desemba 11, katika ukumbi wa shule ya sekondari Chato Mhandis Charles kabeho amesema, ili kukabiliana na changamoto ya ongezeko la wanafunzi katika shule za msingi na sekondari wilayani humo, nivyema kila Mtumishi wa serikali akawajibika kwa nafasi yake bila kusukumwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Eliud Mwaiteleke amewatahadharisha watumishi wazembe  katika eneo hilo kuwa waanze kujiengua mapema kwani awamu hii haihitaji watumishi wavivu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chato Eliud Mwaiteleke

Baadhi ya madiwani walioapishwa wamempongeza Mkuu wa wilaya ya Chato kwa hatua ya kufuta likizo zote kwa watumishi wa umma, kwani itasaidia kupunguza changamoto katika shule za msingi na sekondari  kwa muda mchache uliosalia.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chato Christian Manunga

Akifunga kikao cha baraza hilo Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Christian Manunga amewataka watumishi wa umma na madiwani walioapishwa kushirikiana kwa pamoja ili kuwaletea maendeleo wananchi.

 

 

 

 

Post a Comment

0 Comments