TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

NAIBU WAZIRI WA NCHI OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA) MHE. MWITA WAITARA AHIMIZA USAFI WA MAZINGIRA GEITA

 

 Naibu Waziri  wa  Mazingira  Mhe, Mwita Waitara

Naibu waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mwita Waitara ametoa amewataka watendaji wa serikali Mkoani Geita kuhakikisha wanasimamia kwa uwezo wao suala la usafi wa mazingira ili kuepukana na mlipuko wa magonjwa mbalimbali yanayoweza kujitokeza.


Mhe, Waitara akiwa katika ziara yake ya kikazi katika halmashauri ya Mji wa Geita Mkoani Geita  Desemba 28,2020 ametoa maagizo hayo katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita nakusema kuwa viongozi wengi nchini wamekuwa wakijisahau kusimamia majukumu yao nakusema kuwa suala la usafi wa mazingira nikila siku nasiyo kila mwisho wa mwezi kama ilivyokuwa.

Naibu Waziri  wa  Mazingira  Mhe, Mwita Waitara akiwa na viongozi wa mkoa wa Geita katika Dampo la taka ngumu halmashauri ya mji wa Geita.



Kwa upande wake Afisa usafi na mazingira wa halmashauri ya mji wa Geita Bw Aloys Mutayuga amemhakikishia naibu waziri kuwa ataendelea kusimamia shughuli za usafi wa mazingira kwa uwezo wake wote ili kuepukana na changamoto ya magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu na magonjwa mengine.


Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandis Robert Gabriel ameiomba wizara ya mazingira kupitia kwa naibu waziri Mhe, Waitara kuendelea kushirikiana kwa pamoja na ofisi yake ili kudhibidi visababishi vya magonjwa ya mlipuko mkoani Geita kwakuwa shughuli nyingi za wakazi wa eneo hilo ni uchimbaji wa madini uya dhahabu ambao unatumia kemikali ambazo ni hatari kwa usalama wa maisha ya watu kama zisipo hifadhiwa vizuri.

 

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandis Robert Gabriel

Wananchi Mkoani Geita wamepongeza hatua ya Naibu waziri kwa kuendelekea kuhimiza suala la usafi wa mazingira kwakuwa idadi kubwa ya watu nanajisahau sana katika suala la usafi wa mazingira ikiwemo kujenga nakutumia vyoo bora katika makazi na maeneo ya biashara zao.

Post a Comment

0 Comments