TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI YA DHAHABU MKOANI GEITA WATAKIWA KUZINGATIA USAFI WA MAZINGIRA ILI KUEPUKA MAGONJWA YA MLIPUKO.

 

Wachimbaji na wachenjuaji wadogo wa madini ya dhahamu

 Mtaa wa Mgusu mjini Geita


Wachimbaji na wachenjuaji wa madini ya dhahabu  katika Mtaa wa Mgusu Halmashauri ya Mji wa Geita Mkoani Geita wametakiwa kuzingatia usafi wa mazingira ili kuepukana na Magonjwa ya Mlipuko wakati huu wa msimu wa  mvua.

 

Akizungumza na kituo hiki Mkuu wa Idara ya Mazingira na Usafi kutoka katika Halmashauri ya Mji wa Geita Ndg. Aloyce Mtayuga amewataka wananchi katika eneo hilo kuwa mstari wa mbele katika kuahakikisha Usafi unafanyika kila mara bila kushurutishwa.

 


Mtayuga amesema zoezi la usafi katika baadhi ya maeneo imekuwa ni changamoto hali ambayo imekuwa ikiwapa Muda mwingi wa kuzungukia Maeneo yenye changamoto hususani katika migodi ya wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu.

Kaimu Mwenyekiti wa Mtaa huo Bw Benson Kinaamila ametumia fursa hiyo kuwasisitiza wakazi wa eneo hilo kuendelea kuzingatia usafi hususani katika maeneo yao ya uchimbaji na uchenjuaji wa madini ya dhahabu.

 


Baadhi ya wakazi wa eneo hilo wamesema ukosefu wa sehemu maalumu ya kuhifadhi taka ngumu ndiyo  changamoto kwao yakushindwa kuhili masuala ya usafi wa mazingira kwakuwa shughuli zao zilazalisha taka kwa wingi.

Post a Comment

0 Comments