TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

WAWEKEZAJI WAONESHWA FURSA YA KUWEKEZA KWENYE MIRADI YA USAFI WA MAZINGIRA


Kaimu Ofisa Afya na Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale mkoani Geita Bw Ntiliyo Ezekiel 


Wawekezaji nchini wameshauriwa kuwekeza katika miradi ya usafi wa mazingira ili kuweza kuepukana na uchafuzi wa mazingira ambao unaweza kupelekea mlipuko wa Magonjwa yatokanayo na uchafuzi wa mazingira.


Wito huo umetolewa na kaimu Ofisa Afya na Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale mkoani Geita Ntiliyo Ezekiel wakati akiongea na kituo hiki, Katika kampeni ya usafi wa mazingira katika mamlaka ya mji mdogo wa Kharumwa na maeneo mengine ya wilaya hiyo.

 

Ezekiel ameeleza kuwa kuna umuhimu mkubwa wa wawekezaji kuwekeza katika miradi ya usafi wa mazingira, kwani kwa kufanya hivyo itawanufaisha kiuchumi na kuisaidia serikali kuokoa fedha inayotumika kugharamia matibabu na kununua vifaa tiba ili kudhibiti Magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu na kichocho.

 

Kwa mjibu wa ofisa huyo, amekieleza chombo hiki cha habari kuwa, Tafiti za wataalamu wa maswala ya Afya zinaonesa kuwa, Kila ikiwekezwa Dola Moja katika mradi wa usafi wa Mazingira, huokoa zaidi ya Dola Kumi ambazo zingeenda katika manunuzi ya Dawa na vifaa Tiba kwa ajili ya kugharamia matibabu ya Magonjwa yatokanayo na uchafuzi wa mazingira.

 

Ameendelea kufafanua kuwa katika wilaya hiyo wawekezaji wengi huwekeza katika sekta ya madini sekta ambayo imetajwa kuwa ni kichocheo kikubwa Cha uchafuzi wa vyanzo vya maji na mazingira kwa ujumla.

 

Mmoja Kati ya wekezaji katika Sekta ya Madini na mwanasiasa Nguri wilayani humo, ambaye hakupenda jina lake litajwe, amekiambia chombo hiki Cha habari kuwa, wanashindwa kutekeleza matakwa ya kisheria ya utunzaji wa mazingira kutokana na mitaji midogo waliyonayo hivyo kushidwa kujenga miundombinu imara ya kulinda na kuhifadhia taka.


Ameongeza kuwa katika swala la kuwekeza katika miradi ya uhifadhi wa mazingira, ni fulsa nzuri, hivyo amewataka wawekezaji mbalimbali kuitazama katika jicho pevu, ili jamii iweze kunufaika kupitia uwekezaji huo ambao unatanjwa kuwa na tija kwa makundi yote.


Baadhi ya wananchi wa wilaya hiyo akiwemo Samson kinuno ameeleza kuwa,  shughuli za uchenjuaji wa dhahabu ni kichocheo kikubwa cha uchafunzi wa vyanzo vya maji, hali ambayo inaweza kusababisha Magonjwa Nyemelezi yanayoweza kupelekea mlipuko wa Magonjwa yatokanayo na matumizi ya maji yasiyo salama.


Mwananchi huyo aliendelea kujipambanua kuwa Wakazi wengi wa wilaya hiyo wanategemea maji ya visima vya asili na Yale ya ziwa Viktoria hivyo kuendelea kufanya uchafuzi katika vyanzo vidogo vinavyopokea maji kutoka chanzo kikubwa ambacho ni ziwa Vikitoria, inaweza kuhatarisha afya za watu wengi hivyo kuomba serikali kuchukua hatua ili kudhibiti mazingira.

 


Post a Comment

0 Comments