TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

WAZIRI WA MAJI JUMAA AWESO AMEWASIMAMISHA KAZI MENEJA NA KAIMU WAKE GEITA DC

Muonekano wa Mradi wa Maji wa Chankorongo Geita Dc

Waziri wa Maji Mhe, Jumaa Aweso amewasimamisha kazi meneja na kaimu meneja wa huduma za maji mjini na vijijini RUWASA wilaya ya Geita kwa kushindwa kusimamia vizuri mradi wa maji wa Nyakagomba na Chankorongo uliyopo wilayani humo.

Waziri wa Maji Jumaa Awezo akizungumza katika Mradi wa Maji wa Nyakagomba

Akiwa katika ziara  ya siku moja ya kukagua miradi hiyo  wilayani Geita Waziri Aweso amewasimamisha kazi Meneja wa Huduma za maji mjini na vijijini RUWASA wilayani Geita Sani Sonda na kaimu wake Omega Agustino kwa kushindwa kusimamia miradi hiyo vizuri.

Kushoto Mbunge wa Jimbo la Busanda akizungumza na Waziri wa Maji Jumaa Aweso

Mbunge wa jimbo la Busanda wilayani  Geita  Tumain Magesa amesema mradi wa Nyakagomba umetumia zaidi ya shilingi milioni 600 na ulianza kutekelezwa mwaka 2009 bila mafanikio yoyote mpaka sasa.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandis Robert Gabriel akizungumza Jambo 

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandis Robert Gabriel amesikitishwa na utendaji mbovu wa wahandis hao nakutumia fursa hiyo kuwakumbusha watumishi wengine kuwa wakati huu ni wakati wa kazi.

 


Post a Comment

0 Comments