TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

GGML KINARA KATIKA KUSAIDIA JAMII MIRADI YA MAENDELEO GEITA


Makamu Rais wa kampuni ya Geita Gold Mine Limited (GGML) Mhe. Saimon Shayo akitoa salaam za mgodi kwa mgeni rasmi kwenye sherehe ya ufunguzi rasmi wa maonesho ya nne ya teknolojia na uwekekezaji kwenye sekta ya madini Geita Septemba 22,2021

Makamu Rais wa kampuni ya Geita Gold Mine Limited (GGML) Mhe. Saimon Shayo akizungumzia mchango wa sekta ya madini mkoani Geita amesema kwa kipindi cha miaka mitatu mgodi wa GGML umechangia zaidi ya shilingi bilioni 30 kwa lengo la kusaidia jamii katika shughuli za maendeleo.


 Mhe. Saimon Shayo (Makamu Rais wa kampuni ya Geita Gold Mine Limited - GGML) akitoa shukrani za mgodi kwa serikali kuweka mzingira mazuri ya uwekezaji mbele ya mgeni rasmi kwenye sherehe ya kufungua rasmi maonesho ya nne ya teknolojia na uwekekezaji kwenye sekta ya madini
Geita leo Septemba 22,2021

"Tunaishukuru  serikali   kwa kuendelea   kuleta   sheria   mpya   ambazo   ziemeendelea  kuwatambua  wazawa,  lakini  kipekee  niishukuru  serikali   kwa namna  ambavyo   imeendelea  kutambua  mchango  wa kampuni  ya GGML  katika suala la kurejesha faida wanayopata kwa jamii inayozunguka mgodi huo (CSR)" alisema  Simon  Shayo Makamu wa Rais wa kampuni ya Geita Gold Mine Limited - GGML). Makamu wa Rais wa mgodi GGML ameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Mama Samia Suluhu Hassan (Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) kwa  utekelezaji wa  sheria mpya zilizofanyiwa marekebisho mwaka 2017 zinazo husu washiriki wazawa katika sekta ya madini (Local content).

Rais wa shirikisho la vyama vya wachimbaji wadogo wa madini Tanzania (FEMETA) Mhe.John Bina akitoa salaamu za wachimbji wadogo kwa mgeni rasmi kwenye sherehe ya kufungua rasmi maonesho ya nne ya teknolojia na uwekekezaji kwenye sekta ya madini Geita leo Septemba 22,2021
Rais wa shirikisho la vyama vya wachimbaji wadogo wa madini Tanzania (FEMETA) Mhe.John Bina akitoa salaam za wachimbji wadogo alisema kuwa wachimbaji wataendelea kulipa kodi za serikali huku akiiomba serikali kuweka msukumo kwenye taasisi za kifedha ziweze kuwakopesha mikopo ya masharti nafuu.
Viongozi wa serikali, taasisi za umma na binafsi pamoja na wananchi wakiwa wameketi sherehe ya kufungua maonesho ya nne ya Teknolojia na uwekezaji kwenye sekta ya madini, mgeni rasmi akiwa ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa (MB) 22/9/2021


Post a Comment

0 Comments