TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

WARATIBU WA KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI NI WATETEZI WA HAKI ZA WAANDISHI WA HABARI

Waratibu wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa UTPC na IMS wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kufuatilia na kutoa taarifa za vitendo vya ukiukwaji haki za waandishi wa habari. Walio kaa kuanzia upande wa kulia kwako ni Seif Mangwangi (Mratibu Arusha Press Club), Wakili Jones Sendodo, Mr. Rashwart (International Media Support Zimbabwe), Domiciana Mwalusito (Mratibu Singida Press Club) na Mr. Victor Maleko (Ofisa Program wa Mafunzo, Utafiti na Machapisho-UTPC), waliosimama mstari wa kwanza kushoto ni Mratibu Geita Press Club, Pemba Press Club, Dodoma Press Club, Rukwa Press Club, Tabora Press Club, Iringa,Mwanza na Pwani na wengine wa mikoa yote kama Mara, Shinyanga, Zanzibar, Kagera, Manyara, Kilimanjaro,na Simiyu

WARATIBU wa Klabu za Waandishi wa habari nchini Tanzania wametakiwa kuongeza jitihada za kufuatilia matukio ya ukiukwaji wa haki za binaadam dhidi ya waandishi wa habari kwani wao ni watetezi wa haki za binadamu na wamefundishwa kutoa taarifa juu ya matukio na vitendo vya ukiukwaji haki za binadamu kwa waandishi ikiwemo kunyimwa haki ya kupata taarifa kwaajili ya kuchukuliwa hatua.


Akifungua mafunzo ya siku tatu kwa waratibu hao jana Jijini Dodoma, Ofisa Programu Mafunzo, Utafiti na Machapisho kutoka Muungano wa Klabu za waandishi wa habari Tanzania (UTPC) Victor Maleko amesema waandishi wa habari wamekuwa wakikabiliana na vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu na kukwamisha utendaji wao wa kazi wa kila siku.


Pichani ni Waratibu wa Klabu za waandishi wa habari wakipata mafunzo ya utetezi wa haki za binadamu hususan kufuatilia matukio ya ukiukwaji haki za waandishi wa habari. Kutoka upande wa kulia kwako ni Mratibu wa Mbeya, Dodoma, Zanzibar, Mwanza, Manyara, Kagera, Pemba, Iringa, Singida, Arusha, Morogoro na Geita Press Club.

Ofisa huyo kutoka UTPC amesema UTPC kwa ushirikiano na shirika la IMS Denmark wameingia mkataba wakusimamia haki za waandishi wa habari dhidi ya vitendo na matukio ya ukiukwaji wa uhuru wa habari (madhila),  ambayo ni moja ya haki za msingi kwa binadamu yeyote kuwa na haki ya uhuru wa kujieleza, haki ya kupata na kutoa habari na  waratibu kwa kuwa ni kiungo kikubwa wanatakiwa kuongeza juhudi za kutoa taarifa (Report) matukio hayo ili hatua stahiki zichukuliwe kuyakomesha.

Katika picha ni Waratibu wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania wakijadiliana katika makundi wasilisho la kwanza  kutoka kwa Wakili Jones Sendodo wakati wa mafunzo ya kufuatilia na kuripoti madhira kwa waandishi wa habari nchini Tanzania .


Maleko amesema ili kufanikisha zoezi hilo UTPC imekuwa ikitoa mafunzo na midahalo mbalimbali ya ulinzi na usalama kwa mwandishi wa habari ikiwemo waratibu kujengewa uwezo wa kufuatilia madhila dhidi ya waandishi wa habari nchini Tanzania.

Kwenye picha hapo juu alie simama ni Mr. Rashwart kutoka Zimbabwe akitoa mada juu ya namna ya kufuatilia na kutoa taarifa za ukiukwaji wa haki za binadamu kwa waandishi wa habari, waliokaa wote ni waratibu kutoka katika Klabu za waandishi wa habari zilizopo katika kila mkoa nchini Tanzania wakimsikiliza kwa makini na kuandika pointi za msingi kutoka kwa muwakilishi huyo wa IMS Zimbabwe.
"Leo mko hapa kwaajili ya kujengewa uwezo wa namna bora ya kufuatilia ukiukwaji wa haki za kupata taarifa na uhuru wa habari ikiwemo madhila dhidi ya waandishi wa habari, tunaamini baada ya mafunzo haya mtarudi kazini mkiwa mko vizuri kutoa taarifa (Report) matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu kwa waandishi wa habari”, amesema Victor Maleko.

Pichani ni Waratibu wa Klabu za Waandishi wa habari nchini Tanzania wakifuatilia kwa ukaribu zaidi mkufunzi ambae pia ni wakili Bw. Jones Sendodo wakati akitoa mada mahususi kuhusu sheria za kitaifa na kimataifa juu ya haki za binadamu na haki za waandishi wa habari katika kutekeleza majukumu yao ya kukusanya, kuchakata, na kutoa habari.

Akiwasilisha mada kuhusu uhuru wa kujieleza na akitumia uzoefu wake  Wakili John Sendodo amesema ili kuweza kutambua haki za msingi za binadamu ni vyema kujua haki za kimataifa na namna nchi zingine zimekuwa zikitekeleza haki hizo.

Pichani ni Waratibu wa Klabu za Waandishi wa habari nchini Tanzania wakifuatilia kwa ukaribu zaidi mkufunzi ambae pia ni wakili Bw. Jones Sendodo wakati akitoa mada mahususi kuhusu sheria za kitaifa na kimataifa juu ya haki za binadamu na haki za waandishi wa habari katika kutekeleza majukumu yao ya kukusanya, kuchakata, na kutoa habari.
                                  

Pia amesema kumekuwepo na mikataba ya kimataifa kuhusu haki za binadamu ambayo Tanzania ni miongoni mwa mwanachama wake hivyo ni vyema waratibu wakaelewa na kujua mipaka yao wakati wa kuripoti matukio hayo.

Kwenye picha hapo juu alie simama ni Mr. Rashwart  mwakilishi wa IMS kutoka Zimbabwe akitoa mada juu ya namna ya kufuatilia na kutoa taarifa za ukiukwaji wa haki za binadamu kwa waandishi wa habari, waliokaa wote ni waratibu kutoka katika Klabu za waandishi wa habari zilizopo katika kila mkoa nchini Tanzania wakimsikiliza kwa makini na kuandika pointi za msingi .

Kwa upande wake mwakilishi kutoka shirika la IMS Zimbabwe, Rashweat Mukundu ametoa uzoefu wake kuhusu madhila yanayotokea Zimbabwe na kuwataka waratibu hao kuwa makini wakati wa kuchambua madhila hayo kwa kuwa wanaoyafanya na wao hutumia akili nyingi sana.

“Nchini Zimbabwe waandishi wa habari wanafanyiwa sana madhila lakini kama hauko makini unaweza usibaini ukweli wa tukio lililotokea, hivyo mbinu mbalimbali zinahitajika ili kuweza kubaini,”amesema.


Kwenye picha ni Bw. Seif Mangwangi Mwenyekiti wa Waratibu wa Klabu  za waandishi wa habari Tanzania ambae pia ndiye  Mratibu wa Arusha Press  Club-APC  (kulia) akitafakari mafunzo ya haki za binadamu hususan waandishi wa habari na kushoto kwake ni Mr. Hafigwa mratibu wa Morogoro Press Club.

Pia amewataka waratibu kuripoti haraka matukio ya madhili pindi yanapotokea ili kurahisisha upatikanaji wa mwandishi aliyetendewa tukio husika lakini pia kufanya uchambuzi wa kina na kubaini ukweli ili kuepuka mgogoro usiokuwa wa lazima na mamlaka za kiserikali.


Katika picha ni Waratibu wa Klabu za Waandishi wa Habari wa klabu ya Kigoma Press Club Dianna Rubanguka (kushoto), na Mwajuma Kitwana mratibu wa Mtwara Press Club (kulia)wakiwa kwenye mafunzo ya namna ya kuripoti madhira yanayo wakumba  waandishi wa habari Tanzania.


Post a Comment

0 Comments