TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

MIAKA 60 YA UHURU WITO UMETOLEWA KWA KILA MMOJA KUFANYA KAZI KAMA VILE ATAKUFA LEO

Katika picha ni Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Rosemary S. Senyamule wakati akiwaongoza  na kuhutubia wananchi wa mkoa wa Geita kuelekea kwenye kilele cha maadhimiosho ya miaka 60 ya Uhuru  na miaka 59 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 9 Disemba 2021

Na Mwandishi Wetu, Geita

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Rosemary Senyamule ametoa wito kwa wananchi wa mkoa huo kufanya kazi kwa bidii kwa lengo la kujiletea maendeleo, " Nitoe wito  kwenu kila mmoja afanye kazi kama vile atakufa leo  ili uhuru huu uendelee kuleta maana  na kuonesha thamani na maendeleo hivyo kila mmoja afanye kazi kwa kujituma na kwa bidii kwani uchumi haukui kwa kulala usingizi" amesema.

Amesema hayo leo tarehe 8 Disemba ,2021 wakati akiwaongoza wananchi wa mkoa wa Geita kwenye maadhimiosho ya miaka 60 ya Uhuru  na miaka 59 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hafla iliyofanyika  katika ukumbi wa GEDECO mjini Geita ambapo pia amewataka viongozi wa dini katika mkoa huo kuwaunganisha watanzania ili kulinda umoja na mshikamano uliopo nchini kama tunu ya taifa ili kuenzi amani na mshikamano uliopo nchini.

vile vile Mkuu wa Mkoa Mhe. Senyamule amesema baada ya Baba wa Taifa viongozi waliofuata waliendelea kuboresha miundo mbinu ya bara bara na miundombinu nyingine za kutolea huduma za  afya kwa wananchi kwa lengo la kukuza uchumi wa taifa.

Hata hivyo amewataka wananchi wake pamoja na kufanya kazi kwa bidii wachangamkie fursa ya kupata chanjo kwa hiari ya UVIKO 19 ili kujikinga na maradhi hayo ambayo hivi sasa tupo kwenye wimbi la nne la ugonjwa huo.

Picha ya wananchi waliohudhuria hafla ya maadhimiosho ya miaka 60 ya Uhuru  na miaka 59 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hafla iliyofanyika  katika ukumbi wa GEDECO mjini Geita 8/12/2021 

Nae Mkuu wa wilaya ya Geita Mhe. Wilson Shimo ametumia nafasi hiyo kuwataka wananchi kudumisha umoja pamoja na kufanya kazi kwa bidii kama ngao ya kujitegemea kwenye wakati huu ambapo Taifa limitimiza miaka 60 ya Uhuru.


Pichani  ni wananchi  na viongozi wa serikali waliohudhuria hafla ya maadhimiosho ya miaka 60 ya Uhuru  na miaka 59 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hafla iliyofanyika  katika ukumbi wa GEDECO mjini Geita 8/12/2021 

"Akina mama wanakopesheka maana wanaongoza kwa urejeshaji wa mikopo kwenye halmashauri, haya ni matunda ya Uhuru wa Tanzania". Amesema Mhe. Martha Mkupasi Mkuu wa Wilaya ya Chato. Aidha Mhe. Martha Mkupasi amesema kuwa kuelekea miaka 60 ya Uhuru nchini kumekuwa na ongezeko la viongozi wanawake na akabainisha kuwa akina mama ni nguzo imara na ndio viongozi kwenye ngazi ya familia.

Picha ya wananchi waliohudhuria hafla ya maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru  na miaka 59 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hafla iliyofanyika  katika ukumbi wa GEDECO mjini Geita 8/12/2021 
Mkuu wa Wilaya Mbogwe Mhe. Mhandisi Charles Kabeho  amesema hali ya usafiri zamani ilikuwa ya shida lakini kwa sasa watu wanasafiri kwa urahisi  kutokana na kuimarishwa kwa miundo mbinu  hapa nchini. " Kila Mtanzania anawajibu wa kufikiri namna gani ya kulitumikias taifa lake la Tanzania ili kupata mafanikio", Mhandisi Kabeho.
Kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Nyang'hwale Katibu tawala wa wilaya ndugu Fabian Yinza amewapongeza viongozi wa awamu zote za uongozi hapa nchini tangu uhuru kwa kuliletea Taifa maendeleo. " Bidhaa zitashuka bei sana kutokana na uwepo wa reli ya kati na vijana wengi watapata ajira kupitia uwepo wa reli ya hii ya kati." Amesema.

Kwenye picha ni wananchi  na maofisa wa serikali ya mkoa wa Geita waliohudhuria hafla ya maadhimiosho ya miaka 60 ya Uhuru  na miaka 59 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hafla iliyofanyika  katika ukumbi wa GEDECO mjini Geita 8/12/2021 

Bi. Rhoda Simon, Mwalimu mstaafu aliyezaliwa  tarehe 9 Disemba, 1961 amemshukuru Mungu kwa uhai hadi anashuhudia nchi ikiadhimisha miaka 60 ya Uhuru. Amsema miaka ya nyuma Geita mjini kulikuwa na shule moja tu ya sekodari ya wasichana  lakini sasa shule za sekondari ni nyingi na ziko karibu jambo linalopelekea wanafunzi kutembea umbali mfupi kufika shuleni.
Maadhimisho haya yameenda sambamba na Dua na Sala maalum ya kuwaombea viongozi na Taifa kwa ujumla ili liendelee kuwa na amani  na kuwa nchi yenye mafanikio kiuchumi.

Post a Comment

0 Comments