TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

OFISI YA MKUU WA MKOA GEITA YATAMBUA USHIRIKI WA GEITA PRESS CLUB-GPC KWENYE MAONESHO




Katika picha kutokea upande wa kushoto kwako ni Renatus B.D Masuguliko (Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari  Mkoa wa Geita-Geita Press Club GPC) akipokea cheti/hati kutoka kwa Paul Zahoro (Afisa habari wa Mkoa wa Geita) kulia kwaniaba ya Mkuu wa Mkoa Geita, hati ya  kutambua ushiriki wa  Geita Press Club -GPC kwenye maonesho ya Nne ya Teknolojia na Uwekezaji katika Sekta ya Madini yaliyoanza tarehe 16 hadi 26 Septemba 2021 katika uwanja wa kituo cha uwekezaji Bombambili mjini Geita, aliyesimama katikati ni Beatus Stephen Bihigi (Mratibu-GPC) akishuhudia zoezi la kukabidhi hati hiyo kwa GPC.

Na Mwandishi Wetu, Geita
Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Geita (Geita Press Club-GPC) imepokea hati ya kutambua ushiriki wake kwenye maonesho ya Nne ya Teknolojia na Uwekezaji katika Sekta ya Madini yaliyoanza tarehe 16 hadi 26 Septemba 2021 katika uwanja wa kituo cha uwekezaji Bombambili mjini Geita kutoka kwa Ofisa habari wa Mkoa wa Geita Paul Zahoro kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Rosemary S. Senyamule leo tarehe 08/12/2021.

Katika picha kutokea upande wa kushoto kwako ni Renatus B.D Masuguliko (Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari  Mkoa wa Geita-Geita Press Club GPC) akipokea cheti/hati kutoka kwa Paul Zahoro (Afisa habari wa Mkoa wa Geita) kulia kwaniaba ya Mkuu wa Mkoa Geita, hati ya  kutambua ushiriki wa  Geita Press Club -GPC kwenye maonesho ya Nne ya Teknolojia na Uwekezaji katika Sekta ya Madini yaliyoanza tarehe 16 hadi 26 Septemba 2021 katika uwanja wa kituo cha uwekezaji Bombambili mjini Geita, aliyesimama katikati ni Beatus Stephen Bihigi (Mratibu-GPC) akishuhudia zoezi la kukabidhi hati hiyo kwa GPC
Maonesho ya  Teknolojia na Uwekezaji katika Sekta ya Madini  yaliasisiwa  rasmi katika Mkoa wa Geita kwa mara ya kwanza mwaka 2018, na yamekuwa yakifanyika kila mwaka huku Geita Press Club-GPC  ikishiriki kikamilifu kwenye maonesho hayo  kwa miaka yote 2018, 2019, 2020 na 2021 kwa awamu ya nne.
Picha ya Cheti cha kutambua ushiriki wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Geita (Geita Press Club-GPC) kwenye Maonesho ya Nne ya Teknolojia na Uwekezaji katika Sekta ya Madini kilichotolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita kwa Waandishi wa habari mkoa wa Geita leo 8 Disemba, 2021

Marabaada ya kupokea hati hiyo ya kutambua ushiriki wa GPC kwenye maonesho ya  Nne ya Teknolojia na Uwekezaji katika Sekta ya Madini kutoka kwa Ofisa habari wa Mkoa wa Geita Bw.Paul Zahoro aliekabidhi hati hiyo kwa Mwenyekiti wa  Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Geita Bw. Renatus B.D.Masuguliko,  ameishukuru Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita kwa kuonesha kwa vitendo kutambua ushiriki wa Klabu ya Waandishi wa habari kwenye maonesho ya nne ya Teknolojia na Uwekezaji katika Sekta ya Madini, na kuahidi waandishi wa habari kuendelea kutoa ushirikiano katika shughuli mbali mbali za mkoa huo wa Geita.

Post a Comment

0 Comments