TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

WANANCHI SENGEREMA WASHANGILIA TAA ZA BARABARANI

Mwonekano wa barabara na baadhi ya Wananchi wa Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza wakishangilia taa za barabarani.

Na Anna Ruhasha, Mwanza.

Wananchi wilayani Sengerema mkoani mwanza wameiponge serikali  ya awamu ya sita  kwa kuweka taa za barabarani  ambapo kilikuwa kilio chao cha muda mrefu husasani kwa wafanyabiashara   , mama ntilie na bodaboda.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti  Vaireth Ndembeto  na Joshua Mabula  wamesema kuwa kwa sasa wilaya ya Sengerema imegeuka  kuwa Ulaya ndogo  huku wakifanyabishara zao nyakati za usiku bila bugudha.

 Sambamba na Pongezi hizo  kwa serikali y awamu ya sita ya Mh  Rais Samia Suluu  Hasani pia wamempongeza mbunge  wa jimbo la Sengerema Hamis Tabasamu kusimamia vyema  maendeleo ya  Sengerema kuhakisha anatekeleza ahadi alizoziahidi wakati akiomba ridhaa ya kuongoza wananchi wa Sengerema mkoani mwanza.

Kwakweli Mh Tabasamu anafanyakazi na ukiangalia tangu aingie madarakani asilimia kubwa yale aliyotuahidi ametekeleza ,tunamshukuru pia”wamesema.

Hata hivyo taa hizo mpaka sasa zimefungwa zaidi ya kilometa mbili huku zikiendelea kufungwa kwa mji wa Sengerema.


Mwisho

Post a Comment

0 Comments