TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

MBUNGE AWAPA USINGIZI WAFUNGWA

Mbunge Hamis Mwagao Tabasamu (kulia) akikabidhi magodoro na blangeti kwa naibu waziri wa mambo ya ndani.

Na Anna  Ruhasha, Mwanza. 

Jamii  imeombwa   kujitoa   kusaidia   makundi yenye  uhitaji   ikiwa ni pamoja na kutenga muda wa  kujitoa       kutembelea  wafungwa  magerezani   na  kutoa  misaada  kulingana  na uwezo ili   wajione hawajatengwa  na jamii  waliyotoka. 

Wito  huo   umetolewa  na  Naibu  Waziri  wa  mambo  ya ndani   Jumanne  Sagini    wakati   akikabidhi  magodoro 170  na   blangeti  170 na  taa za  sola  3 zilizotolewa  na   mbunge  wa jimbo  la sengerema   kwa wafungwa  wa  gereza  la kasungamile  wilayani  Sengerema Mkoani  Mwanza.  

Naibu Waziri akimkabidhi magodoro mkuu wa magereza mkoa wa Mwanza Justine Kaziulaya kwaajili ya Wafungwa. 

Aidha    mkuu wa  magereza  mkoa  wa Mwanza   Justine  Kaziulaya   ameshukuru  kwa  Kitendo  cha mbunge kujitoa kutoa sadaka hiyo  na kuhidi  kusimamia na kuhakikisha kila  mfungwa na mahabusu wanapata. 

Mbunge wa jimbo la Sengerema  Hamisi  Tabasamu amesema   kwake  siyo msaada bali  ni sadaka  kulingana  na ombi  la wafugwa kwake baada ya kutembelea gereza  hilo na kukuta wanala chini ya Sakafu  na kukosa blangeti za kujifunika.

Ameongeza kwa kusema kuwa yeye kama muumini  aliguswa na changamoto hiyo iliyomsukuma kutumia sehemu ya msahahara wake kiasi cha zaidi ya laki nane  zilizotumika  kununua  hao ikiwa ni magodoro ,sola na Blanketi. 

Mh waziri nilikuja katika gereza hili kama sehemu ya ziara yangu kwenye tasisi wakati naongea na wafungwa walinieleza hawana vilalio magodoro na blangeti,niliguswa maana na mimi ni binadamu naweza kuja kufungwa hapa  nikamuuliza mkuu wa gereza hili jumla ya wafungwa akaniambia wapo 170 na mimi nimeleta magodoro 170 na blangeti 170 na hii ni Sedaka siyo Msaada”amesema Tabasamu. 

Mbunge Tabasamu akikabidhi magodoro na Blanketi kwa Naibu Waziri Mambo ya ndani ya Nchi Jumanne Sagini kwaajili ya Wafungwa. 

Aidha  , mwenyekiti   wa  chama cha mapinduzi CCM  wilayani  Sengerema   Maki  Agustine   amesema   mbunge  Tabasamu  amekuwa  akijitoa kwa jamii   Hususa katika kuwaudumia wagonjwa pamoja na wafungwa siku za ijumaa kila wiki hivyo kama chama kitaendelea kumuunga mkono.

 Wakati huo huo  Naibu Waziri  amekabidhi  tofari  zenye   thamani   ya shilingi milioni 17  kwa jeshi la polisi  Sengerema zilizotolewa  na mbunge  Tabasamu  kupitia  fedha  za  mfuko  wa jimbo  kwaajili ya ujenzi  wa nyumba za maaskari.


MWISHO 

Post a Comment

0 Comments