TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

MKURUGENZI AKANUSHA TAARIFA ZA KUWEPO SHULE KUGEUZWA DANGURO


Mkurungenzi wa Halmashauri ya wilaya  Sengerema Binuru Shekidele akionesha kusikitishwa na taarifa za uwongo kuhusu shule kugeuzwa danguro Sengerema. 

Na Anna Ruhasha, Mwanza. 

Mkurungenzi wa halmashauri ya wilaya ya Sengerema mkoani mwanza  Binuru Shekidele  amekanusha kuwepo kwa shule zinazotumika kama  madanguro.

Ametoa taarifa hizo mbele ya  waandishi wa habari ofisini kwake siku chache baada ya baadhi ya vyombo vya habari pamoja na mitandao  ya kijamii kuandika habari za uwongo kuwepo kwa  vyumba  vya madarasa kutumika kama danguro katika halmashauri ya wilaya ya Sengerema mkoani mwanza.

Aidha , Shekidele  amesema   kuwa picha za shule iliyotajwa  katika mitandao  ya kijamii na chombo cha kuchapisha habari hapa nchini siyo za kweli na kuwaomba wadau wa habari kuzipuuza taarifa hizo.

Katika taarifa zilizotolewa katika mitandao ya kijamii zilionyesha picha ambazo siyo za shule ya msingi Bulunga na hii ndiyo shule ya msingi Bulunga haina changamoto ya milango wala vyumbu kutumika kufanyia ngono kama ilivyosemwa madarasa haya yanafungwa baada ya masomo.

“ Ndugu waandishi wa habari, katika baraza la madiwani  Kuliibuka hoja ya fedha za kapitesheni  kifungu cha asilimia 30 ya  fedha ya ukarabati na nililitolea ufafanuzi  na uzuri  baadhi yenu mlishiriki hicho kikao  sikuzungumza kama  baadhi ya vyombo vilivyochapisha, nilisema kule chifunfu kata ya madaha  palikuwa na Shida ya vyumba vya madarasa  kutofungwa milango lakini kwa sasa hiyo changamoto haipo baada ya kwenda kukagua na katika halmashauri yangu hakuna shule ambayo haina milango wala madirisha na chakushangaa picha za madarasa zilizotumika katika vyombo vilivyoandika uwongo siyo za hapa kwetu naomba wananchi wazipuuze ni zauwongo" amesema Mkurugenzi huyo. 

Nitumie  pia nafasi hii kuwaomba waandishi  wa habari kufuatilia kile kinachokuwa kimesemwa ili kuondoa maswali kwa jamii hususani katika habari hiyo iliyoipotosha jamii kuhusiana na kuwepo kwa madarasa kugeuzwa madanguro wilayani hapa.

Katika  taarifa zilizotolewa katika mitandao ya kijamii zilionyesha picha ambazo siyo za shule ya msingi Bulunga na hii ndiyo shule ya msingi Bulunga haina changamoto ya milango wala vyumbu kutumika kufanyia ngono kama ilivyosemwa madara haya yanafungwa baada ya masomo.

Mwisho 

Post a Comment

0 Comments