TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

RC GEITA AITAKA TRA KUWEKA MAZINGIRA RAFIKI UKUSANYAJI KODI

Pichani  anaesoma aliyevaa suti nyeusi ni Ndositwe Haonga Mkurugenzi wa  mambo ya ndani TRA  Nchini ,muwakilishi wa mkurugenzi wa TRA Nchini. 

Alphonce Kabilondo na Samwel Masunzu ,Geita

Mkuu wa Mkoa wa Geita Martin Shigela ameitaka mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Geita kuweka mazingira  rafiki ya ukusanyaji wa mapato ili kuleta ufanisi mkubwa katika ukusanyaji wa mapato kwa wafanyabiashara Mkoani humo .

Mkuu huyo amesema hayo mjini Geita  wakati akitoa vyeti kwa walipa kodi waliofanya vizuri kwa kulipa kodi bila shuruti mkoani Geita.

 Shigela alisema kuwa serikali kufikia malengo yake lazima kuwepo na mazungumzo na wafanyabiashara pamoja na  kuwapatia elimu badala ya kutumia nguvu katika kukusanya mapato.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigela akimkabidhi vyeti kwa baadhi ya wafanyabiashara waliofanya vizuri katika ulipaji wa kodi bila shuruti,  katikati ni mwenyekiti mpya wa CCM  Mkoa  wa Geita   Nicolaus Kasendamila akishuhudia 

Shigela akisistiza kauli hiyo alisema mamlaka hiyo haina budi  kuweka mazingira rafiki ya ukusanyaji wa mapato  ili kuweza kuleta ufanisi  mkubwa katika kukusanya mapato.

Aidha  Ndositwe Haonga akizungumza kwaniaba ya Kamishina wa mamlaka ya mapato Tanzania TRA alisema, kupitia elimu  ambayo wamekuwa wakiitoa kwa wafanyabiashara, kila mara imeonyesha mafanikio makubwa yameonekana kwenye ukusanyaji wa kodi . 

Pichani Wakwanza kushoto aliyevaa T-shirt nyeupe ni Hashim Ngoda Meneja wa TRA Mkoa wa Geita ,katikati ni Ndositwe Haonga mwakilishi wa Mkurugenzi wa TRA Nchini akikabidhi taulo za kike kwa mkuu wa shule ya wasichana Nyankumbu Girls Jojia Mgashe  

Ndositwe alisema kuwa  mamlaka hiyo imejipanga kuboresha matumizi ya mashine za kielektroniki na ujenzi wa vituo vya  TEHAMA kusajiri walipa kodi na  kubuni vyanzo vya mapato .

Akizungumzia changamoto alisema kuwa baadhi ya wafanyabiashara wasio waadilifu hawatumii mashine za kielektroniki kwa usahihi pamoja na kutotoa risiti hali ambayo inachangia serikali kupoteza mapato 

Meneja wa mamlaka  hiyo Mkoa wa Geita Hashim Ngoda alisema kuwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 walikusanya asilimia 97% na kwa kipindi cha Julai hadi Oktoba 2022  wamefanikiwa kukusanya shilingi bilioni 25 sawa na ufanisi wa asilimia 208% huku lengo likiwa nikukusanya bilioni 35 kwa mwaka 2022/2023 .

Baadhi ya wafanyabiashara waliopatiwa vyeti hivyo akiwemo, Mkurugenzi wa Blue Coast  Investement Bw, Athanas Inyasi wameishukuru serikali kupitia TRA kwa kutoa motisha kwao ambapo wameahidi kuendelea kulipa kodi bila shuruti .

Wakati huo huo katika kuadhimisha wiki ya mlipakodi, Mamlaka ya mapato TRA mkoani Geita imetoa msaada wa  taulo za kike kwa wanafunzi wa shule ya sekondari ya wasichana Nyankumbu Girls ,na msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo vifaa vya shule daftari ,Sabuni miswaki , mafuta ya kujipaka Unga ,Mchele kwenye  vituo vya watoto wenye mahitaji maalumu vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya milioni 6.

Mkuu wa shule ya sekondari Nyankumbu Girls Jojia Mgashe akipokea msaada huo alisema kuwa shule hiyo ina wanafunzi zaidi ya elfu moja huku Sista  Maria Lauda wa kituo cha Moyo wa Huruma kinachomilikiwa na kanisa katoliki akitumia fursa hiyo kuipongeza TRA Mkoa wa Geita .

MWISHO. 

Post a Comment

0 Comments