TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

SERIKALI IMETENGA SHILINGI BILIONI 8 KUTENGENEZA KIVUKO KIPYA CHA NYAKALILO BUCHOSA MWANZA

 

Meneja wakala wa ufundi Tamesa mkoa wa mwanza Alyoce Ndunguru akitoa taarifa ya ujenzi mpya wa kivuko cha nyakalilo Kome

Anna Ruhasha,  Mwanza

Taarifa hizi  zimetolewa na meneja wakala wa Ufundi ( Tamesa )mkoa wa mwanza  Alyoce Ndunguru   …wakati akikabidhi kivuko cha mv  Sabasaba kwa wakazi wa kome ili kupunguza adha ya kutumia kivuko kimoja cha mv komeII ambacho ndicho kilikuwa kikitumika 

Tunafahamu wakazi wa kome kiu yenu ni kuona kivuko kipya lakini kulingana na uhitaji na ombi la mbunge tumeona kwanza  tulete kivuko hiki cha mv sabasaba japo siyo kipya lakini kimefanyiwa matengenezo na maboresho  lakini pia nikikubwa kuzidi hiki cha mv kome II na hii itapunguza changamoto za kubanana kwenye kivuko kimoja kama hilivyokuwa hapo nyuma na vikuko vyote vitafanya kazi “amesema

Baadhi ya viongozi walioshiriki katika mapokezi ya kivuko cha mv sabasaba kabaganga

Aidha ametumia  muda huo kuwaomba wananchi kutunza miundombinu ya vivuko hivyo  kutoka na serikali kutumia fedha nyingi kuvitengeneza.

Baadhi ya wakazi wa kisiwani kome  ,Ajelina kyaruzi na  Johnsen licha ya kupongeza mbunge kuanza kutimimiza baadhi ya ahaadi zake wasema kuwa kilio chao kikubwa nikuona kivuko ambacho watasafiri pasipokuwepo na changamoto za

kunyeshewa  mvua na kusafiri wamesimama.

Tulipo ambiwa tunaletewa  kivuko tuliamasika kuja kama unavyotuona lakini mioyo yetu imesononeka kwasababu kivuko hiki hakina tofauti na mv komeII ambayo tunaitumia  labda ukubwa tu,sisi hatutaki vivuko vya mifugo tunataka vivuko  kama vilivyo vya Busisi ‘wakati wa mvua na jua tuwetuna safiri  kwa raha” wamesema.

Akizungumza na mamamia ya wakazi wa kome Mbunge wa jimbo la Buchosa Erick

Shigongo amewaondoa ofu wapiga kura wake na kusema   anajua huitaji wao wa kivuko kipya wakati wakisubiri miezi 24 kukamilika kivuko kipya  ameona alete mv sababa.

Baadhi ya wananchi walioshiriki

Mimi ni miongoni mwa watu waliozaliwa na kukulia katika maisha ya chini sana najua sana kwanini nimeamuao kutanguliza hiki kivuko  ,kivuko ni sehemu ya haadi zangu lazima kivuko kipya kije tena kikubwa na serikali imeishamlipa..,,bilion mbili,ninacho waomba tupendane tushirikiane tuijenge Buchosa yetu"

Katika hafla hiyo mkuu wa wilaya ya Sengerema Senyi Ngaga ambaye alikuwa mgeni rasmi amewataka wasimamizi wa vivuko hivyo kwenda na muda na kuhakisha wanasafirisha wananchi kwa muda ili Pangea na siyo kuwakalisha vituoni.

Mbunge wa jimbo la Buchosa Erick Shigongo akizungumza na wakazi wa  Buchosa. 

Hata hivyo mwenyekiti wa chama cha mapinduzi Mack Agustine makoye Dm ameongeza kuwa chama kitaendelea kuwapatia ushirikiano viongozi wanaotokana na chama hicho hasa wanaosukuma maendeleo kwa wananchi.

“Chama hakijalala tutawapa ushirikiano viongozi wetu,lakini pia niwaonye mnaonza kampeni chini chini kuna wengine wanagawa baiskeli kwaajiri ya ubunge ,mimi ndiyo mwenyekiti sitawafumbia macho,acheni watu wafanye kazi siyo manenomaneno”amesema Dm.

Picha ya kivuko kipya 


Mwisho

Post a Comment

0 Comments