TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

UWAKA PAROKIA YA BIKIRA MARIA WA FATIMA GEITA, WACHAGUANA.

Na Urban Epimark, GEITA. 

Umoja wa Wanaume Wakatoliki Tanzania (UWAKA) ngazi ya Parokia ya Bikira Maria wa Fatima, Jimbo Katoliki la Geita leo wamewapata viongozi wapya watakao simamia na kuongoza umoja huo kwa kipindi cha miaka mitatu  kuanzia mwaka 2023 hadi 2026.

Parokia ya Bikira Maria wa Fatima, Jimbo Katoliki la Geita.

Uchaguzi huo ambao ni muendelezo wa chaguzi za Halmashauri ya Walei kiparokia katika Jimbo, chini ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania-TEC unajumuisha pia viongozi wa vyama vingine vya kitume pamoja na wale wa Jumuiya ndogo ndogo, ulifanyika leo kwenye kumbi za Parokia ya Bikira Maria wa Fatima mjini Geita.

Msimamizi wa uchaguzi huo Katekista Simon Pauline aliwaambia wajumbe wa mkutano huo ulioshirikisha wawakilishi kutoka mitaa  7 kati ya 10 ya parokia hiyo na pia kigango kimoja kati ya viwili vilivyopo kwamba,


Mwenyekiti aliyetetea nafasi yake wa UWAKA ngazi ya Parokia ya Bikira Maria wa Fatima, Jimbo Katoliki la Geita Bw Salvatory Kazaula (pichani) anae tokea Mtaa wa GESECO akiongea na Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa UWAKA baada ya kumchagua tena kuwa Mwenyekiti wao leo November 05, 2022

"Uchaguzi wa viongozi wa vyama vya kitume pamoja na jumuiya ndogo ndogo huwa kampeni haifanyiki bali ni kwa kupitia sala na maombi kwa Mungu Roho Mtakatifu ambae kwa uweza wake huwachagua viongozi wa Walei kuwaongoza" alisema.

Mkutano huo wa uchaguzi ngazi ya parokia hiyo,  ulioenda sambamba na chaguzi za vyama vingine vikiwemo Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA), Vijana Wakatoliki Tanzania (VIWAWA), Chama cha Lejio Maria na kile cha Wazee Wastaafu cha Mt Augustino.


Katibu Mkuu Mpya wa UWAKA Parokia ya Bikira Maria wa Fatima, Jimbo la Geita Bw Beatus Mazezere (anae ongea) ambae anatokea Mtaa wa Msalala Road akitoa shukrani zake kwa wajumbe wa Mkutano wa UWAKA kwa kumchagua baada ya kukamilika uchaguzi wa UWAKA ngazi ya Parokia leo November 05, 2022.

Mwenyekiti aliye chaguliwa kuiongoza UWAKA, Parokia ya Bikira Maria wa Fatima Bw Salvatory Kazaula (aliye tetea nafasi yake) aliwashukuru wana UWAKA wote kwa kutimiza wajibu wao wa kuchagua uongozi mpya ngazi ya parokia na kusema hiyo ni nguvu mpya.

"Namshukuru sana Mungu leo kwa kutupatia viongozi wapya wa UWAKA ngozi ya parokia kwani tuna amini ni kwa uweza wa Mungu mwenyewe. Kuanzia leo UWAKA haitabaki tena nyuma kwa kazi za kitume hivyo tufungue ukurasa mpya kiutendaji" alisema Mwenyekiti wa UWAKA.


Msimamizi wa Uchaguzi wa UWAKA ngazi ya Parokia ya Bikira Maria wa Fatima, Jimbo Katoliki la Geita, Katekista Simon Pauline (pichani) akiwashukuru wajumbe wa Mkutano Mkuu wa UWAKA baada ya kufanikisha uchaguzi wa UWAKA leo November 05, 2022

Nae Katibu Mkuu mpya wa UWAKA aliye chaguliwa ambae anatokea Mtaa wa Msalala Road Bw Beatus Mazezere aliwashukuru wajumbe wa mkutano mkuu wa uchaguzi wa UWAKA kwa imani yao walio onesha  kwake hadi kumchagua na kutoa ahadi kwa Mwenyekiti wa UWAKA wa Parokia hiyo Bw Salvatory Kazaula kwamba atafanya  kazi kwa bidii na kujituma ili kuhakikisha UWAKA inasonga mbele.

Uchaguzi mkuu wa viongozi wa Kamati Tendaji ya Halmashauri ya Wakei Parokia ya Bikira Maria wa Fatima, Jimbo Katoliki la Geita unatarajiwa kufanyika  jumamosi ijayo November 12, 2022 na viongozi wa vyama vya kitume waliochaguliwa leo wakiwemo UWAKA ni wajumbe wa mkutano huo wa uchaguzi.


Safu mpya ya uongozi wa UWAKA, Parokia ya Bikira Maria wa Fatima, Jimbo Katoliki la Geita walio chaguliwa ni Mwenyekiti, Bw Salvatory Kazaula kutoka Mtaa wa GEDECO (wa tatu kutoka kushoto shati la damu ya mzee) akifuatiwa kulia kwake na Katibu Mkuu mpya wa UWAKA Bw Beatus Mazezere kutoka Mtaa wa Msalala Road (wa pili kushoto) na kisha Mtunza Hazina (aliye chaguliwa tena nafasi hiyo) Bw Lucas Mazubesi (kushoto) kutoka Kigango cha Nyamalembo. Wengine kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa UWAKA Bw Dominick Itare (wa kwanza kulia) akifuatiwa na Naibu Mweka Hazina Bw Gidius Shekanabo kutoka Mtaa wa Msufini (T-shirt ya bluu bahari) na Makamu Mwenyekiti wa UWAKA (aliye tetea nafasi yake) Bw George Robert kutoka mtaa wa GEDECO (mwenye koti)


Msimamizi wa uchaguzi wa UWAKA ngazi ya Parokia ya Bikira Maria wa Fatima, Jimbo Katoliki la Geita Katekista Simon Pauline (katikati) akisaidiana na mjumbe wa Mkutano huo wa UWAKA ambae ni Katibu wa UWAKA kutoka Mtaa wa Katoma Bw Patrick Faida (kushoto) wakiandaa karatasi za kura tayari kwa uchaguzi huo. Pichani mwanzo kulia ni Katibu wa muda wa mkutano huo Bw Dominick Itare (mwenye T-shirt damu ya mzee )


Wajumbe wa mkutano mkuu wa uchaguzi wa UWAKA ngazi ya Parokia ya Bikira Maria wa Fatima, Jimbo Katoliki la Geita wakiwa kwenye ukumbi tayari kwa uchaguzi leo November 05, 2022


Mwisho.

Post a Comment

0 Comments