TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

VIONGOZI WA KLABU IWENI WABUNIFU: MAKAMU WA RAIS-UTPC

Viongozi wa Press Clubs za Kigoma,  Mara, Kagera, Geita na Simiyu pamoja na waratibu wakiwa kitika mafunzo ya Uongozi na Usimamizi wa fedha yaliyoandaliwa na Umoja wa Klabu za waandishi wa Habari Tanzania (Union of Tanzania Press Clubs-UTPC) jijini Dodoma leo November 2,2022.

Na Mwandishi wetu,  Dodoma.

Makamu wa Rais wa Muungano wa klabu za waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) Pendo Mwakyembe ametoa wito kwa viongozi wa Klabu zote za Waandishi wa habari kuwa wabunifu katika kutekeleza majukumu yao ikiwa ni pamoja na kubuni vyanzo vya mapato ili kuweza kuwa na Klabu imara zenye tija kwa wanachama wake, jamii na taifa kwa ujumla. 

Amebainisha hayo wakati akifungua mafunzo ya uongozi na usimamizi wa fedha kwa viongozi wa klabu kutoka mikoa ya Geita, Kigoma, Kagera, Mara, na Simiyu yanayoendelea jijini Dodoma kwa siku tatu mfurulizo kuanzia leo November 2 hadi 4,2022 lengo ni kuwaongezea  ujuzi na maarifa ya Uongozi na Usimamizi wa fedha ili kuleta ufanisi wa kiutendaji katika Klabu zao ili kuendana na Kasi mpya ya UTPC inayongozwa na kauli mbinu isemayo "Moving UTPC from good to great" .

Amesisitiza  viongozi wa ngazi za juu katika Klabu wanapaswa kuwa na mshikamano na mahusiano mazuri wao wenyewe kwanza na kisha kwa wanachama wao wote huku wakizingatia  miongozo ya UTPC  ili Klabu zisiwe kikwazo kwa  wafadhili mbali mbali wenyenia ya kufanya kazi na Waandishi wa Habari Tanzania.


Wakwanza kulia ni Veronica Modest Mwekahazina Mara Press Club,Beatus Stephen Bihigi Mratibu Geita Press Club,Merabu Birakashekwa Mjumbe wa Kagera Press Club,Mbeki Mbeki Mwenyekiti Kagera Press Club,Editha Edward Muwekahazina GPC na Prosper Kwigize Mjumbe wa Kigoma Press Club wakifuatilia Mafunzo ya Uongozi na Usimamizi wa fedha jijini Dodoma leo November 2,2022.

"Kiongozi yeyote wa Press Club asiyeweza kubuni walau chanzo cha mapato ndani ya muda wa kipindi cha miezi mitatu au mitano, anapaswa kujitathimini kwakweli” alisema Mwakyembe.

Kwa upande wake afisa Progamu wa mafunzo utafiti na machapisho wa UTPC Victor Maleko alisema mafunzo hayo yanalenga kuwaandaa viongozi wa Press Clubs nchini Tanzania kutoka kwenye hali ya kuwa tegemezi bali Klabu zifanyike msingi imara wa UTPC ili ziweze kubeba ndoto ya kuihamisha UTPC kutoka kuwa bora hadi kuwa Bora  zaidi.

"Niwaombe Viongozi wa Klabu zote tubadilike  kifikra, Let's move from Comfort zone katika utendaji ili tuboreshe ufanisi wa klabu zetu na UTPC kwa ujumla” alieleza Maleko.


Renatus Masuguliko Mwenyekiti wa Geita Press Club-GPC akichangia hoja wakati wa Mafunzo ya Uongozi na Usimamizi wa fedha jijini Dodoma leo 2 November,2022. Wakwanza kulia ni Novatus Lyaruu Katibu Mkuu Mtendaji Geita Press Club,Frank Kasamwa Mwenyekiti Simiyu Press Club,Mwajabu Hoza Katibu Mkuu Kigoma Press Club na Raphael Okelo Kaimu Mwenyekiti Mara Press Club mwisho kushoto. 

Akichangia mawazo yake kwa niaba ya washiriki wa Mafunzo haya Renatus Masuguliko ambaye ni Mwenyekiti wa Geita Press Club-GPC aliipongeza UTPC kwa kuendesha mafunzo hayo na kwamba yatasaidia kuimarisha mifumo ya uongozi na Usimamizi wa fedha, mambo ambayo yamekuwa chanzo cha migogoro mingi ya  klabu nyingi hapa nchini.

"Mafunzo haya nimazuri sana, tunaahidi kubadilika kwani mambo mengine tulikuwa hatujui na baadhi yetu nimafunzo ya mara ya kwanza" alisema Masuguliko. 


Kuanzia upande wa Kushoto katika picha ni Diana Rubanguka Mratibu wa Kigoma Press Club, Audax Mutasingwa Mratibu wa Kagera Press Club, na Paul Mussa Mratibu wa Simiyu Press Club wakimsikiliza kwa makini Makamu wa Rais-UTPC Pendo Mwakyembe akifungua Mafunzo kwa viongozi wa Klabu.


Mwisho.

Post a Comment

0 Comments