TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

WASABATO WAMLILIA RAIS SAMIA KUPISHANA NA FURSA ZA AJIRA SERIKALINI.

Rais Samia akitoa Tuzo kwa muasisi wa kanisa la Waadventista Wasabato wa mkoa wa Dodoma leo November 19, 2022

Na Urban Epimark,  DODOMA

Kanisa la Waadventista Wasabato wa mkoa wa Dodoma leo limeadhimisha Jubilee ya miaka 50 ya Utume na Huduma tangu kuanzishwa kwake na kumwomba Rais Samia awasaidie kuondoa changamoto tatu kubwa zinazo wakabili.

Rais Samia ambae alikuwa Mgeni Rasmi katika Jubilee hiyo, kanisa hilo limemweleza changamoto za kubinywa uhuru wao wa kuabudu siku za jumamosi ambapo waamini wao hushindwa kuhudhuria usahili wa ajira na mitihani siku hiyo na hivyo kuzikosa fursa za ajira zinazo tolewa.

Rais Samia Suluhu Hassan akikaribishwa na chipukizi wa Kanisa la Waadventista Wasabato katika ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma kwa kupigiwa salute ya heshima leo November 19, 2022

"Mhe Rais, kanisa la Waadventista Wasabato linazo changamoto tatu kubwa kwa wafuasi wetu kukosa nafasi za ajira serikalini na kwingineko kwa vile waandaaji wa usahili hupanga kuwaita wasahiliwa  siku za jumamosi ambapo ni siku yetu ya kumwabudu Mungu" ilisema sehemu ya taarifa ya kanisa hilo iliyosomwa  mbele ya Rais Samia leo katika ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma. 

Rais Samia Suluhu Hassan akikaribishwa katika ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma na viongozi pamoja na kamati ya maandalizi ya Jubilee ya miaka 50 ya Utume na Huduma ya kanisa la Waadventista Wasabato wa mkoa wa Dodoma iliyofanyika leo November 19, 2022. Aliyevalia gauni la bluu ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndg Christina Mndeme.

Changamoto zingine ni kutoheshimika siku ya Jumamosi ambayo ni siku rasmi ya Wasabato kuabudu na kumtukuza Mungu kama ilivyo kwa madhehebu mengine ya wakristo na waisalamu siku zao zinaheshimika na pia kuomba kupatiwa wataalamu wabobezi wa tiba ya afya kwa hospitali zao.

Katika hotuba yake aliyoitoa na kurushwa moja kwa moja na vyombo vya habari leo asubuhi November 19, 2022 kutoka jijini Dodoma, Rais Samia ambae alikuwa Mgeni Rasmi katika Jubilee hiyo alilishukuru kanisa hilo kwa jinsi wanavyoiasaidia serikali katika malezi ya watoto na vijana hapa nchini na kusaidia kudumisha maadili ya utamaduni pamoja na mila za kitanzania.

Sehemu ya wageni na washiriki katika tukio la Jubilee ya miaka 50 ya Utume na Huduma ya kanisa la Waadventista Wasabato wa mkoa wa Dodoma wakiwa katika ukumbi wa Jakaya Kikwete wakifuatilia matukio mbalimbali wakati Rais Samia Suluhu Hassan alipokuwa Mgeni Rasmi leo November 19, 2022

Halikadhalika Rais Samia ameutaka uongozi pamoja na maaskofu wa kanisa hilo halikadhalika viongozi wote wa madhehebu mengine ya dini hapa nchini kufikisha ujumbe kwa wafuasi wao wa kutunza mazingira kwa kupanda miti na kuitunza ili kurejesha uoto wa asili na kusaidia upatikanaji wa maji na mvua za kutosha za misimu.

Awali akimkaribisha Rais Samia ili azingumze na wafuasi wa kanisa hilo walio furika katika ukumbi wa Jakaya Kikwele jijini Dodoma, Askofu Mkuu wa Jimbo la Kaskazini wa Kanisa hilo Askofu Mark Marekana alimshukuru Rais Samia kwa Upendo na Ukarimu wake kwa watanzania kwa kuimarisha kwa kiwabgo cha juu huduma za Elimu na Afya hapa nchini pamoja na ujenzi wa miundombinu mingine ikiwemo madaraja na viwanja vya ndege.

Baadhi ya wajumbe wa kamati ya maandalizi ya Jubilee ya miaka 50 ya Utume na Huduma ya kanisa la Waadventista Wasabato wa mkoa wa Dodoma pamoja na wageni wengine wakifuatilia kwa makini hotuba na buradani mbalimbali zilizokuwa zikiendelea katika ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma leo November 19, 2022

Pia Askofu huyo alimwombea kheri nyingi Rais Samia katika uongozi wake kwani Tanzania imeshuhudia kuwa na Amani na Ushirikiano mkubwa baina ya watanzania na majirani zake wote na kutoa ahadi kwamba kanisa hilo litaendelea kutoa ushirikiano kwake kwa muda wote.

Kanisa la Waadventista Wasabato liliaaza rasmi hapa nchini mwaka 1903 katika wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro na kuenea kidogo kidogo kuelekea Musoma mkoani Mara na kufika hadi mkoani Dodoma kunako mwaka 1972 ambapo leo ndio maadhimisho ya Jubilee ya miaka 50 ya Utume na Huduma katika mkoa wa Dodoma. 

Vijana wa chipukizi wa kanisa la Waadventista Wasabato wa mkoa wa Dodoma pamoja na washiriki wengine wakiwa katika ukumbi wa Jakaya Kikwete wakati wa Jubilee ya miaka 50 ya Utume na Huduma ya kanisa hilo mkoani Dodoma wakifuatilia kwa makini Hotuba ya Mgeni Rasmi ambae alikuwa Rais Samia Suluhu Hassan leo November 19, 2022

Rais Samia akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati ya wanawake wa maandalizi ya Jubilee ya miaka 50 ya Utume na Huduma ya kanisa la Waadventista Wasabato wa mkoa wa Dodoma leo November 19, 2022

Rais Samia akipatiwa maelezo ya mchoro wa ujenzi wa kanisa jipya la Waadventista Wasabato litakalokuwa na uwezo wa kuingiza watu 750 kwa wakati mmoja litakalojengwa mtaa wa Uhindini jijini Dodoma leo November 19, 2022

Rais Samia akiondoa kitambaa kama ishara ya kuzindua ujenzi wa Mnara wa Jubilee ya miaka 50 ya Utume na Huduma ya kanisa la Waadventista Wasabato wa mkoa wa Dodoma leo November 19, 2022

Rais Samia akiagana na waamini pamoja na wananchi walio hudhuria eneo la uzinduzi wa Mnara wa Jubilee ya miaka 50 ya Utume na Huduma ya kanisa la Waadventista Wasabato wa mkoa wa Dodoma leo November 19, 2022

Mwisho.

Post a Comment

0 Comments