TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

KANISA LA FPCT GEITA LIMETOA MSAADA KWA WAFUNGWA

Askofu wa kanisa huru la kipentekoste Tanzania (Free Pentecostal Church of Tanzania -FPCT) jimbo la Geita David Nzumbi akimkabidhi msaada wa wafungwa kwa Mkuu wa Gereza la Wilaya ya Geita Mrakibu mwandamizi wa Jeshi la Magereza SSP Jovin Bujwina, alie vaa jaketi la dark blue wengine ni viongozi wa kanisa hilo na Maofisa wa Jeshi la Magereza wakishuhudia. Wakwanza upande wa kushoto ni Kirian Ndaikeje(Shemasi), Vincent Ntale (Mzee wa Kanisa), Justina John (Katibu UWW Jimbo la Geita),Deus Mwondi (Mwalimu wa watoto), Martha Nzumbi (Mke wa Askofu FPCT Jimbo la Geita), Joram Kidaga (Shemasi) na Mch. Naiman Mtae (alivalia kaunda suti)

Na  Alphonce Kabilondo,Geita 
KANISA huru la kipentekoste Tanzania (FPCT) jimbo la Geita Mkoani hapa limetoa msaada wa sabuni , sukari ,mafuta ya kupikia ,mchele pamoja na Ng’ombe mmoja kwa wafungwa wa gereza la Wilaya ya Geita kwaajili ya kuwawezesha kusherekea Sikukuu ya Kristmas  na mwaka mpya 2023.
Askofu wa kanisa hilo Mch. David Nzumbi akikabidhi msaada huo amesema kuwa  msaada huo umegharimu zaidi ya shilingi  milioni moja lengo likiwa ni kuwawezesha wafungwa kusherekea Sikukuu hizo kwa kuwa nao ni sehemu ya jamii .
Askofu huyo alisema kuwa msaada huo umetokana  na michango ya waumini wa kanisa kufuatia utaratibu wa kanisa hilo  wa kila mwaka  kuwa tembelea wafungwa waliopo gerezani na kufanya nao ibada, kuwajulia hali na kuwatia moyo na kuwasaidia mahitaji mbalimbali .
“Tumekuja kufanya ibada na wafungwa leo na kuwasaidia mahitaji mbalimbali mafuta,sukari,sabuni, mchele , na kitoweo cha Ng’ombe kwaajili ya Sikukuu ya Kristmas, tumetimiza maandiko matakatifu  tunaamini kuwa nao ni sehemu ya jamii wamo ndani yao watumishi wanamtumikia Mungu" alisema Askofu Nzumbi.

Askofu wa kanisa huru la kipentekoste Tanzania FPCT jimbo la Geita Mch. David Nzumbi akisalimiana na Mkuu wa Gereza la wilaya ya Geita 
Mrakibu mwandamizi wa Jeshi la Magereza SSP Jovin Bujwina, alie vaa jaketi la bluu wengine ni viongozi wa kanisa hilo na Maofisa wa Jeshi la Magereza wakishuhudia.

Justina John katibu wa wanawake wa kanisa la FPCT jimbo la Geita alisema kuwa katika kusherekea Sikukuu ya Kristmas  tumeungana na waumuni wenzetu kuja kuwajulia hali wafungwa na kuwapatia mahitaji mbalimbali .
Aidha Mkuu wa gereza la Wilaya ya Geita mrakibu mwandamizi wa jeshi la magereza SSP Jovin Bujwina amelipongeza kanisa la FPCT Jimbo la Geita kwa msaada huo na ambapo ameshauri madhebu mbalimbali ya dini kuiga mfano wa kanisa hilo la FPCT Geita .
Mkuu huyo aliongeza kuwa waumini wa kanisa hilo wamefanya jambo jema  la kuwasadia wafungwa hao na kwamba hawastahili kunyanyaswa wala kutengwa kwa kuwa nao bado ni sehemu ya jamii.

Baadhi ya Vitu mbalimbali vilivyo tolewa na Kanisa la FPCT Geita kwa Wafungwa wa Gereza la Geita, ikiwemo kitoweo cha Ng'ombe na Mchele kwaajili ya kusherehekea siku kuu ya krismasi na Mwaka mpya 2023.


MWISHO  

Post a Comment

0 Comments