TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

MWENYEKITI WA JUMUIYA YA CCM ATATUA KERO ZA KADI NA MIHULI

Mwenyekiti wa jumuiya ya CCM wilayani Sengerema mkoani mwanza Jackson Mazinzi akikabidhi kadi na mihuli kwa baadhi ya viongozi kata Nyatukala

Na Anna Ruhasha, Mwanza. 

Jumla ya matawi ya   Jumuiya ya wazazi CCM 197  wilayani sengerema  mkoani Mwanza yameondokana na ukosefu wa mihuli na kadi za jumuiya hiyo baada ya Mwenyekiti wa wilaya Jacksoni Mazinzi  kuchonga mihuli  na kununua kadi zaidi ya 2000 na kuigawa bure kwa kila tawi kwa lengo la kuondoa changamoto hiyo iliyodumu kwa muda mrefu bila kupatiwa ufumbuzi na  viongozi walio pita.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ziara  yake na kamati ya utekelezaji amesema mihuli na kadi za jumuiya ni sehemu ya ahaadi yake  kwa wajumbe ambapo walimtaka akishika kijiti cha uongozi  awatatulie changamoto hizo. 

“Wakati nagombea mlinitaka nitatue changamoto za kadi na mihuli na mimi nimefanya hivyo mnakumbuka niliahidi kadi elfu moja lakini kulingana uhitaji nitatoa  kadi bure 2250 kwa kata zote 47 za wilaya ya Sengerema niliahiadi natekeleza”alisema.

Kwa upande wake katibu wa jumuiya ya wazazi wilaya ya Sengerema  Jamali  Athuman  alitumia  ziara hiyo kuwakumbusha wajumbe na wananchama wa jumuiya hiyo kufanya kazi kwa ushirikiano na viongozi waliopo madarakani na kuendelea kusemea mazuri yanayofanywa na Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan hususani ujenzi wa vyumba  vya madarasa unaoendelea katika wilaya hiyo.

 Hata hivyo baadhi ya viongozi kamati tekelezaji waliongozana na Mwenyekiti  Dickson Mtaka na  Josephat Makoli…walishauri kuwa ziara hiyo isiishie katika jumuiya ya wazazi badala yake kila jumuiya iwafikie wanachama na viongozi ili kuwasikiliza na kutatua kero zao kuliko kusubiri wakati wa uchaguzi.


Mwisho

Post a Comment

0 Comments