TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

SHIRIKA LATOA MSAADA WA BAISKELI 500 KWA WANAFUNZI WA KIKE GEITA

Wilson Shimo Mkuu wa Wilaya Geita (Koti ya bluu) akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Geita kuipongeza Plan International wakati wa hafla ya ugawaji baiskeli 500 kwa Wanafunzi wa kike. Pembeni yake pande zote ni Maafisa walioambatana nae kwenye hafla hiyo mjini Geita. 

 Na  Alphonce Kabilondo ,Geita

SHIRIKA la kutetea haki za watoto, plan International limetoa msaada wa  baiskeli miatano 500 kwa lengo la kuwasaidia wanafunzi wakike wanaotembea umbali mrefu kwenda .

Mkurugenzi wa mradi  wa kuwawezesha wanafunzi wa  wakike wenye rika  balehe  kuendelea na masomo KAGIS Nicodemas Gachu amesema kuwa mradi huo unaotekelezwa kwa ufadhili wa serikali ya watu wa Canada kwa kushirikiana na Shirika la plan International  kwa kipindi cha miaka mitano .

Wilson Shimo Mkuu wa wilaya Geita (alievaa koti la rangi ya bluu) akikata utepe ishara ya kufungua hafla iliyoandaliwa na shirika la Plan International, hafla ya kugawa baiskeli kwa watoto wa kike Wanafunzi wanaotembea kwa miguu umbali mrefu kwenda Shule. 

Alisema kuwa kati ya baiskeli hizo 300 zitagawanywa kwa wanafunzi wakike wanaotembea umbali mrefu kwenda shule  katika Mkoa wa  Geita na 200 kwa wanafunzi wa Mkoa wa Kigoma wanaotembea umbali mrefu.

Katika picha alievalia shati la drafti akitabasamu baada ya Mkuu wa wilaya Geita kukata utepe  ni Mkurugenzi wa Miradi wa Shirika la Plan International Bw Peter Mwakabwale . 

Mradi huu utawawezesha wanafunzi wakike  wenye rika balehe kuendelea na masomo   na kuwa epusha na vishawishi vya kufanya mapenzi katika umri mdogo na kusababisha  mimba za utotoni ''alisema Mkurugenzi huyo .

Mkuu wa Wilaya Geita Wilson Shimo akikabidhi baiskeli kwa mmoja wa Wanafunzi wa kike waliopatiwa baiskeli na Shirika la Plan International, upande wa Kushoto (alievaa saa nyeusi) ni Mkurugenzi wa Miradi wa Shirika la Plan International Peter Mwakabwale akishuhudia zoezi la kugawa baiskeli kwa watoto wa kike ili kuwanusuru na adha ya kutembea umbali mrefu kwa miguu wakati wa kuenda Shule. 

  Mkurugenzi wa miradi ya shirika la plan International Nchini Peter Mwakabwale alisema kuwa shirika la plan  limekuwa likifanya kazi mkoani Geita toka mwaka 2000. na kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ya Elimu, kuzuia ajira hatarishi kwa Watoto, Usafi wa mazingira pamoja na ulinzi kupitia ufadhili wa Serikali ya Watu wa Canada (GAC) kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania, 

  

Mkuu wa Wilaya Geita Wilson Shimo akikabidhi baiskeli kwa mmoja wa Wanafunzi wa kike waliopatiwa baiskeli na Shirika la Plan International, upande wa Kushoto (alievaa saa nyeusi) ni Mkurugenzi wa Miradi wa Shirika la Plan International Peter Mwakabwale akishuhudia zoezi la kugawa baiskeli kwa watoto wa kike ili kuwanusuru na adha ya kutembea umbali mrefu kwa miguu wakati wa kuenda Shule. 
"Shirika la Plan International linaunga mkono juhudi za serikali, chini ya mradi huu wa KAGIS ambapo baiskeli 2,000 zitanunuliwa na kusambazwa kwa wanafunzi wa kike mpaka kukamilika kwa mradi huo pia mbali na mradi huo shirika hilo limekuwa likitekeleza miradi mbalimbali ikiwemo Elimu ,kuzuia ajira hatarishi kwa Watoto ,Usafi wa mazingira "alisema Mkurugenzi huyo .

Baadhi ya Wazazi na Wanafunzi waliohudhuria hafla ya ugawaji baiskeli kwa watoto wa kike Geita. 

Awali Mkuu wa Wilaya ya Geita Wilison Shimo aliyekuwa amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Geita kwenye  hafla hiyo  alliipongeza shirika  na serikali ya watu wa Canada kwa  wa mradi huo huku akisisitiza baiskeli hizo zitumike kwa malengo yaliyokusudiwa badala ya kugeuka kuwa mali ya wazazi wa wanafunzi hao .

Baadhi ya Wanafunzi waliokabidhiwa baiskeli kama wanavyoonekana katika picha hii wakiwa na nyuso za furaha. 

Mwanafunzi wa shule ya sekondari Bung'wangoko Mkoani Geita  Aneth Komanya akatumia fursa hiyo kulishukuru shirika hilo kwa msaada huo na kuahidi kusoma kwa bidii na kufikia malengo yao huku mwanafunzi Keflini wa shule ya sekondari Ihanamilo akisema kuwa awali walikuwa wakitembea umbali mrefu kwenda shule hivyo baiskeli hizo zitawasaidia kwenda shule na kufika kwa wakati na kuwaepusha na vishawishi njiani kutoka kwa mafataki .


 MWISHO

Post a Comment

0 Comments