TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

WAFANYAKAZI ZAID YA 40 WAPOETEZA AJIRA MGODI WA UCHAKATAJI DHAHABU WA ILILIKA GEITA

 

Na  Mwandishi wetu, Geita. 

WAFANYAKAZI zaidi ya 40  wamepoteza ajira  kutokana na miundombinu ya kuchakata dhahabu  iliyopo katika Kijiji cha Ililika wilaya na Mkoani Geita  kusimamishwa na Ofisi ya Madini Mkoa  wa Geita kutokana na kudaiwa kuibuka mgogoro  kati ya waliokuwa wabia wanaodai  kuchangia kujenga  miundombinu katika mgodi huo wa uchakataji madini.

Akithibitisha hivi karibuni kuwepo kwa hatua hiyo mwekezaji mzawa  wa Leseni hiyo  Elias Lukasi Kivuyo   anadai  kutoshirikishwa  na baadhi ya maamzi  yanayokinzana  na uhalisia  yanayotolewa na ofsisi ya madini mkoa wa Geita  kumekuwa kunachangia  kuibuka  kwa baadhi  ya migogoro, hatua ambayo wafanyakazi wa kutwa yaani vibarua 40 watapoteza fursa za kufanya kibarua,kumuathiri yeye mwenyewe kiuendeshaji pamoja na kodi za Serikali.

Kivuyo anadai kuwa kabla ya ofisi ya madini mkoa wa Geita kuchukua hatua iliyochukuliwa kulikuwepo na ubishani   kuhusu badhi ya miundombinu waliyojenga pamoja  na aliyekuwa mbia wake Richard Kasubi baada ya mkataba kati yao wa kufanya kazi uliomalizika  mwaka jana 2022, na hivyo kuhitaji majadiliano au tafasiri ya kisheria hatua mabayo imefanywa na  ofisi ya madini Mkoa kama kumshinikiza ili akubali  hatua anayoipinga akidai kuna dalili za uonevu.

Mabishano hayo yalihusu  miundombinu iliyojengwa  kwa ubia wakati wakiwa wabia  kufanyiakazi ndani ya Leseni ya Uchimbaji  ya Elias Lukasi Kivuyo baada ya kupata leseni ya ubia ya uchakataji madini kwa kufanyia katika eneo la Elias Lukasi Kivuyo na aliyekuwa mbia wake Kasubi ibakie  kuwa mali ya nani baada ya mkataba kutokana na mkataba husika kutosema chochote juu ya kipengele hicho mara baada ya mkataba kumalizka.

Kivuyo anadai kuwa alimkaribisha  aliyekuwa mbia wake Richard Kasubi kuingia nae ubia kufanya kazi katika leseni yake ya uchimbaji  katika kitalu chake  kilichopo katika kitongoji cha Ililika ambapo kupitia leseni ya ubia wao  ya kuchakata madini Processing License  No:0006 wakiwa wabia.

Aidha kwa ajili ya kuchakata dhahabu  eneo la Ililika  katika kata ya Nyarugusu wilayani Geita na Richard Kasubi aliamua kufungua shauri la madai  katika mahakama ya mwanzo Busanda /Nyarugusu mwaka jana 2022 akidai ni  madai yanayotokana na kuwekeza  katika ubia wao baada ya mkataba wao kumalizika.

Hata hivyo baada ya kuanza kulisikiliza   shauri hilo mahakama hiyo ilibaini kuwa haikuwa na mamlaka ya kusikiliza kutokana na kiwango cha shilingi milioni 75 kilichokuwa kimefunguliwa kwa mdai kuwa mahakama ya mwanzo haikuwa na  mamlaka ya kulisikiliza  na hivyo kulifuta kwa kumuelekeza mdai Richard Kasubi akafungue shauri hilo katika mahakama ya wilaya hatua ambayo haikutekelezwa  na mdai kwa wakati huo.

Kutokana na kutokea kwa mazingira hayo mmiliki wa kitalu kulipokuwa kunafanyika uchakataji kwa ubia   Elias Lukasi Kivuyo anadai nae aliwasilisha katika mahakama hiyo ya Mwanzo ya Busanda /Nyarugusu madai dhidi  ya aliyekuwa mbia wake  Richard Kasubi kuendelea  kufunga  moja ya chumba  ambacho  kilidaiwa kuhitajika kutumika kwa ajili ya shughuli zingine za mgodi kilichokuwa kinatumika  kwa ubia kabla ya mkataba kumalizika. 

Kufuatia hatua hiyo Mahakama ya mwanzo Busanda /Nyarugusu  Oktoba 30 mwaka 2022 ilitoa agizo  kwa mwenyekiti wa kitongoji cha Ililika katika kata ya Nyarugusu ilipo leseni na miundombinu ya kuchakatia  dhahabau inayobishaniwa  asimamie utekelezaji wa kufungua chumba husika na kisha Mahakama iairifiwe kuhusu Utekelezaji huo.

Hata hivyo baada ya utekelezwaji huo Richard Kasubi aliyekuwa mbia wa Elias Lukasi Kivuyo alianza kulalamikia hatua hiyo akidai chumba kilichovunjwa alikuwa  amehifadhia kaboni zake  kutokana na kuvunjwa kufuli na kuwekwa kufuli jingine wakati yeye akiwa hayupo madai yanayopingwa na Elias Lukasi Kivuyo kuwa hatua hiyo ilikuwa ni utekelezwaji wa agizo la Mahakama iliyotolewa kwa mwenyekiti wa kitongoji cha Ililika Paulo Luhende na tayari mkataba ulikuwa umesha malizika wa ubia wao.

Akizungumzia  madai hayo mwenyekiti wa kitongoji cha Ililika Paulo Luhende anakiri kutekeleza agizo hilo ikiwa ni amri halali ya mahakama ya mwanzo Busanda/Nyarugusu ililyotolewa Oktoba 30 mwaka jana 2022 na kuwa baada ya kuitekeleza  alirejesha taarifa ya utekelezaji huo kwa  mahakama kuhusu  Utekelezaji huo uliofanyika hadharani.

Hata hivyo kwa upande wake yeye kama aliyekuwa  amepokea jukumu la kutekeleza amri hiyo ya mahakama anasema wakati wa kutekeleza  jukumu hilo walikuta hakuna kitu chochote cha thamani  ndani ya chumba hicho isipokuwa malapa lapa  ya mifuko ya sandarusi na uchafu unaotokana na chumba hicho kufungwa kwa muda mrefu na hapakuwepo na kaboni kama inavyodaiwa.

Awali akiuzngumzia  madai hayo Richard Kasubi alisema kuwa alikuwa ameingia katika mgogoro na aliyekuwa mbia wake Elias Lukasi Kivuyo  ambaye waliingia nae Ubia ili kufanya kazi pamoja ambapo walijenga  baadhi ya miundombinu kwa pamoja na ili kufanikisha uendeshaji lakini katika eneo la Elias Lukasi Kivuyo na kupata Leseni ya uchakataji namba 0006 M/S Richard Kasubi &Lukasi Ole Kivuyo Oktoba 16 mwaka 2012 kila mmoja akiwa na hisa ya asilimia 50.

Kasubi aliongeza kudai kuwa tatizo  lilianza baada ya mkataba kukoma wa ubia wao wa leseni ya kuchakata madini  namba PCL 0006 mkataba wao haukuwa umesema lolote  mara baada ya mkataba wao kukoma wa ubia miundombinu itakuwaje hatua ambayo imeibua sintofahamu  hivyo kuhitaji majadiliano au tafasiri ya kisheria na vyombo vya kutoa haki.

Aidha katika hatua nyingine Richard Kasubi anadai kuwa  kuvunjwa kwa chumba anachodai alikuwa amehifadhia kaboni zake hatua anayodai  hakubaliani nayo ya kuvunjwa chumba bila yeye kuwepo   hatua inayozidi kuongeza mvutano zaidi kati yao wakati Elias Kivuyo na Mwenyekiti wa kitongoji cha Ililika Pualo Luhende wakikanusha madai ya Richard Kasubi kuwa hayana ukweli na kuwa utekelezaji huo ulifanyika kwa agizo halali la Mahakama ya mwanzo Busanda/Nyarugusu. 

Kaimu Afisa madini Mkazi mkoa wa Geita Martine Shija amekiri kuwepo  kwa hatua hiyo na mgogoro  huo lakini atalitolea ufafanuzi  baada ya kupata kibali  cha kuzuangumza na wanahabari   atakapokuwa amepta kibali kutoka kwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini. 
                                                              MWISHO.

Post a Comment

0 Comments