TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

MBUNGE FURAHA ATAO FURAHA KWA WALEMAVU: MFANO WA KUIGWA.

Mhe Furaha Matondo akizungumza  katika mkutano wa hadhara wakati akikabidhi viti mwendo kwa watu wenye mahitaji maalumu wilayani sengerema mkoani Mwanza.

Na Anna Ruhasha, Mwanza. 

Mbunge viti maalum mkoa wa mwanza Furaha  Matondo ameitaka jamii kuwalinda na kuwapenda na kuacha kuwanyanyapaa watu wenye ulemavu  ambapo amesema watu hao ni watu kama watu wengine  wanahaki ya kusaidiwa        na kupewa vitendea kazi  na mitaji pia.

Picha ya baadhi ya  viti mwendo kutoka kwa Mhe Mbunge viti maalum mkoa wa Mwanza Bi. Furaha Matondo. 

 Mbunge  Matondo amesema hayo wakati wa zoezi la kutoa viti mwendo  16 wilayani Sengerema  mkoani Mwanza kati ya  viti hivyo, viti  (8) nane vimetolewa kwa walemavu waishio halmashauri ya Buchosa  na  viti nane (8) vilivyo baki vimetolewa kwa walemavu wanaoishi katika halmashauri ya wilaya ya Sengerema.

Aidha, Mhe Matondo amesema anakila sababu ya kutoa viti mwendo hivyo maana vitawasaidi walemavu kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine kwa urahisi.

Baadhi ya wataalamu wa ulemavu wa viungo kutoka  CCBRT wakionyesha jinsi ya matumizi sahihi ya viti mwendo hivyo baada ya kuwapima  na kuhakikisha wanakaa bila bugudha.

“Ndugu zangu  wananchi na walemavu mlioko hapa kwa kuguswa na changamoto mnazozipitia hasa kutoka sehemu mmoja kwenda sehemu nyingine nimetoa viti mwendo 70 kwa baadhi ya walemavu kwa wilaya zote za mkoa wa Mwanza lakini pia na fimbo kwa ndugu zangu vipofu.”

Baadhi ya wazazi na walezi wa walemavu wa viungo vya miguu na macho wakipokea vifaa hivyo wamemshukuru mbunge huyo kwa kutumia sehemu ya mshahara wake kuwasaidi watu wenye uhitaji ambapo wameahidi kuvitunza katika mazingira mazuri.

Picha ya pamoja baadhi ya walemavu waliopokea kwa furaha viti mwendo kutoka kwa Mbunge viti maalum mkoa wa Mwanza.

Nao  baadhi ya watu wenye ulemavu  licha ya kushukuru wameomba viongozi kuiga mfano kwa Mbunge Matondo ambaye amekuwa mfano boro kwa jamii kuwafikia watu wenye uhitaji zaidi.

Mwenyekiti wa  UWT wilayani Sengerema  Jenny Msoga ametumia nafasi hiyo kumshukuru mbunge Furaha Matondo kurudisha furaha kwa watu wenye mahitaji maalum ambapo amesema kuwa  wataendelea kumpa ushirikiano wa kutosha kwani  amekuwa kiongozi wa kusaidia  jamii zenye uhitaji.

Baadhi ya wataalamu wa ulemavu wa viungo kutoka CCBRT wakionyesha jinsi ya matumizi sahihi ya viti mwendo hivyo baada ya kuwapima na kuhakikisha wanakaa bila bugudha.

“Tunakushukuru Mbunge wetu ,tunawashukuru wataalamu kutoka CCBRT kukubali kuambatana  na mama huyu mbunge kuja  kutoa vipimo kwa ndugu zetu kabla hawajapewa viti mwendo hivyo unasifa ya mitano tena mbungeni"  amesema Msoga.

Hata hivyo katika taarifa iliyosomwa na katibu wa UWT Sengerema Rosemary Mwakisalu amesema Mhe Furaha amekuwa msaada mkubwa  wa kujitoa na kuchangia mambo mbali mbali  kwenye jamii na kwenye chama ambapo pia amesha toa shuka kwa wagonjwa katika kituo cha afya Project , amechangia ujenzi wa  mradi wa choo cha  UWT na kununua mashine ya kudurufu (Photocopy machine) katika ofisi ya  UWT Sengerema.

Picha ya pamoja baadhi ya walemavu waliopokea kwa furaha viti mwendo kutoka kwa Mbunge viti maalum mkoa wa Mwanza.


Mwisho

Post a Comment

0 Comments