TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

KAMPUNI KUMWAGA MIKOPO YA VIFAA , VYA KISASA VYA UCHIMBAJI MADINI KWA WACHIMBAJI WADOGO KANDA YA ZIWA

Mkurugenzi  wa biashara na masoko  wa kampuni ya GF TRUCKS & EQUIPMENT Salman Karmali wanne kutoka kulia alievaa suti (mweupe) akikata utepe katika hafla ya ufunguzi wa ofisi mpya ya kampuni hiyo iliyofunguliwa soko kuu la dhahabu mkoani Geita. 

Na  Alphonce  Kabilondo,Geita. 

KAMPUNI ya uuzaji wa vifaa vya kisasa vya uchimbaji madini, mitambo na magari makubwa  GF Trucks & Equipment  imewashauri wachimbaji  madini wadogo  na wakati  mkoani Geita  pamoja na mikoa jirani ya kanda ya ziwa kuunda vikundi ili waweze  kukopeshwa  vifaa vya kisasa vya uchimbaji madini na mitambo.

Mkurugenzi  wa biashara na masoko  wa kampuni  hiyo  Salman Karmali ametoa ushauri huo jana mjini hapa kwenye hafla ya ufunguzi wa ofisi mpya ya kampuni hiyo iliyofunguliwa soko kuu la dhahabu mkoani hapa.

Salman Karmali Mkurugenzi wa biashara na masoko wa kampuni ya GF TRUCKS & EQUIPMENT watatu katikati akiwa ameketi wakati wa hafla ya kuzindua rasmi Ofisi ya GF TRUCKS & EQUIPMENT katika soko kuu la dhahabu mkoani Geita

Mkurugenzi huyo amesema kuwa  kampuni hiyo imeamua kuingia ubia na taasisi za kifedha ili kuwasaidia mikopo ya vifaa vya kisasa na mitambo ya uchimbji madini kwa wachimbaji wadogo na wakati hivyo wachimbaji wadogo na wakati hawana budi kuunda vikundi vya uchimbaji ili waweze kukopesheka.

Alisema  kuwa lengo la kampuni hiyo  kufungua  ofisi mkoani Geita ni kusogeza huduma kwa wachimbaji wadogo hasa wa mkoa huu wa Geita pamoja na mikoa jirani ya kanda ya ziwa huku akiipongeza serikali kwa kuweka mazingira mazuri kwenye sekta ya madini.

Aidha  alisema kuwa mbali na kampuni hiyo kuwakopesha vifaa na mitambo wachimbaji wadogo kadhalika wanakodisha vifaa na mitambo kwa wachimbaji  lengo likiwa ni kuwainua wa chimbaji wadogo wa madini .

Mkurugenzi wa biashara GF TRUCKS kanda ya ziwa aliyevaa T-shirt nyeupe kwenye hafla ya ufunguzi Ofisi ya kampuni hiyo mkoani Geita. 

Tutawafikia wachimbaji wadogo wote kwenye maeneo yao  ya uchimbaji na  kuwapatia elimu ya matumizi ya vifaa vya  kisasa Mkoa wa Geita na mikoa ya jirani ya kanda ya ziwa" alisema Karmali .

Awali katibu  wa chama cha wachimbaji wadogo mkoa wa Geita    (GEREMA)   Golden Hainga akitoa kilio cha wachimbaji wadogo alisema kuwa wachimbaji wengi wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa vifaa vya kisasa vya uchimbaji madini pamoja na mitaji na kutoaminiwa na taasisi za kifedha .

Wachezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Geita Gold wakiwa katika furaha mdamini wao GF TRUCKS & EQUIPMENTS kufungua Ofisi mkoani Geita. 

Alisema kuwa uchimbaji madini kwa kutumia  dhana duni unachangia wachimbaji wengi  kupata uzalishaji mdogo wa madini angali wakitumia  gharama kubwa kuendesha shughuli za uchimbaji wa madini.

Katibu huyo aliongeza kuwa kampuni hiyo imekuja na suluhisho kwa  wachimbaji wadogo ambapo  alitoa wito kwa wachimbaji wadogo mkoani humo   kuchangamkia fursa  ya mikopo ya vifaa na mitambo ya kisasa.

“Wachimbaji wengi mkoani Geita bado wafanya uchimbaji madini kwa kutumia dhana duni kampuni hii imekuja muda mwafaka kwa wachimbaji hususani wa mkoa wa Geita" alisema Hainga.

Mkurugenzi wa biashara na masoko wa kampuni ya GF TRUCKS & EQUIPMENT Salman Karmali wanne kutoka kulia alievaa suti (waliosimama mstari wa mbele-mweupe) katika picha ya pamoja na wadau, viongozi wa Geita Gold na wachezaji kwenye hafla ya ufunguzi wa Ofisi ya kampuni hiyo mkoani Geita. 

Mwenyekiti wa  chama cha wachimbaji wadogo wa madini mkoani hapa GEWOMA  Husina  Mwasimba alisema kilio kikubwa cha wachimbaji wadogo ni ukosefu wa mitaji,  vifaa vya kisasa vya uchimbaji wa madini na hivyo kuiomba kampuni hiyo kuwakopesha vifaa kwa mikopo ya masharti nafuu.

Mwisho. 

Post a Comment

0 Comments