Na Editha Edward-Geita;
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya
Nyang’hwale Hamisi Tsaxara amewapongeza
wajumbe wa mkutano mkuu wa uchaguzi wa umoja wa wanawake Tanzania UWT wilayani
humo kwa utulivu na umakini waliouonyesha katika uchaguzi wa kuwapata madiwani
viti maalumu.
Hamis
ambae ndie alikuwa msimamizi mkuu wa uchaguzi huo alisema hayo mara baada ya
kusoma matokeo ya uchanguzi huo ambapo alisema kuwa wilaya hiyo inakata 15 na tarafa
4.
“Kama tulivyo sema mwanzo hizi ni kura za maoni baada ya hapa kuna
mchakato wa vikao , waliopiga kura katika tarafa ya Bukwimba wagombea walikuwa
wawili, wajumbe waliopiga kura ni 862, kura zilizo haribika 23, kura halali 839
ambapo Magreth James Petro amepata kura 186 na Ester Mabura Sebastian amepata
kura 653” alisema Hamisi.
Katibu
huyo alisema kuwa tarafa ya Msalala
wagombea walikuwa 4 na wajumbe waliopiga kura ni 860, kati ya kura 860
kura zilizoharibika ni 18, na kura halali ni 842. Matokeo Chausiku Masanja Katoto kura 144, Bernadeta Aloyce kura 149,
Salome Method Gwanchele kura 216 na
Grace Lukasi Mavuno 332 na tarafa ya
Nyang’hwale waliopiga kura 862 zilizo
haribika ni 6, kura halali 856; matokeo
Hongera Ibrahimu Luchemba alipata kura 84, Laulensia Jakobo Tome alipata kura
272 na Agnes Matibu Mashimi alipata kura 500.
Tarafa
ya Nyijundu waliogombea ni wawili na
kura zilizo pigwa ni 833 kura zilizo haribika ni 5, kura halali 828;
matokeo Herena Mahona Shija alipata kura 361
na Stella Slivanus Ndenge alipata kura 467; wagombea mmoja mmjoja kila tarafa walioongoza
kwa kura ndio watakao kuwa wawaklishi.
Kwa
tarafa zote nne washindi ni Ester Mabula
Sebastian kutoka tarafa ya Bukwimba,
Grace Lukas Mavuno kutoka tarafa ya Msalala, Agnes Matibu Mashimu kutoka tarafa ya Nyang’hwale,
Stella slvanus Ndege kutoka tarafa ya Nyijudu na mtu watano ni Herena Mahona
Shija uchaguzi huo ulifanyika katika ukumbi wa Malala sekondari.
Picha: Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Nyang’hwale Happines Isack John




0 Comments