Na Theresia C Method,
Kanyasu akichukua
fomu ya ubunge ofisi ya Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Geita
Geita, Juni 30, 2025 – Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini anayemaliza muda
wake, Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, ameonyesha nia ya kuendelea
kulitumikia jimbo hilo kwa kuchukua rasmi fomu ya kugombea ubunge kupitia Chama
Cha Mapinduzi (CCM) kwa muhula mwingine.
Kanyasu amepokea fomu hiyo leo katika
Ofisi ya CCM Wilaya ya Geita kutoka kwa Katibu wa CCM Wilaya, Michael Msuya,
akieleza kuwa ana imani kubwa na mchakato mzima wa ndani ya chama.
Akizungumza mara baada ya kukamilisha
hatua hiyo muhimu, Kanyasu amesema; “Katiba
inaruhusu kupiga kura na kupigiwa kura, hivyo kujitokeza kwa wingi kwenye
kugombea ni ishara nzuri ya chama kuwa hai”
Aidha, Kanyasu ameahidi kuendeleza kazi aliyoianza ya kuleta
maendeleo katika sekta mbalimbali ndani ya Jimbo la Geita Mjini ikiwa atapata
ridhaa ya chama na wananchi kuendelea kuwakilisha bungeni.
Kwa sasa, mchakato wa kuchukua na
kurudisha fomu za kugombea nafasi ya ubunge ndani ya CCM unaendelea huku
wanachama mbalimbali wakiendelea kujitokeza kuwania nafasi hiyo katika maeneo
tofauti ya nchi.

0 Comments