TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

MADIWANI WAIKATAA TAARIFA YA TANESCO SENGEREMA

Kaimu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Sengerema Makoye Sengerema.

Na Anna Ruhasha, Mwanza.

Baraza la madiwani halmashauri ya wilaya Sengerema mkoani Mwanza imeikataa taarifa ya shirika la umeme TANESCO  wilayani humo kwa madai ya kutokidhi vigezo vya taarifa zinazotakiwa katika vikao vya madiwani .

Diwani wa kata ya Tabaruka Mhe Sospiter Busumabu akichangia hoja katika baraza la madiwani baada ya shirika la TANESCO kuwasilisha Taarifa.

Hatua hiyo imekuja baada ya kutolewa hoja na diwani wa kata ya Tabaruka Sospiter Busumabu na kuungwa  mkono na diwani wa kata ya Nyampande  George Kazangu baada ya taarifa hiyo kuwasilishwa na kaimu Meneja wa TANESCO  ambae  hakutaka jina lake litajwe  ambapo taarifa hiyo kukosekana saini ya Meneja TANESCO wilaya ya Sengerema.

 Diwani wa halmashauri ya wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza akichangia hoja kwenye kikao cha baraza la madiwani. 

Aidha,kaimu mwenyekiti wa halmashauri  Mhe Makoye Sengerema alipoliuliza baraza la madiwani baada ya  kaimu meneja kuwasilisha taarifa  hiyo mbele ya kikao cha madiwani , baraza hilo liliikataa taarifa hiyo na kuagiza kwenda kuandaliwa taarifa nyingine itakayo wasilishwa  kwenye kikao kijacho na kujadiliwa upya.

Baadhi ya madiwani  wa halmashauri ya wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza 


Baadhi ya madiwani  wa halmashauri ya wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza 


Mwisho. 

Post a Comment

0 Comments