TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

VALERIA MAKONDA: MAJUKWAA YA WANAWAKE NI SEHEMU MAALUM KUWATOA WANAWAKE KATIKA UMASKINI

Mratibu wa dawati la uwezeshaji wanawake kiuchumi katika halmashauri ya mji Geita Mkoani hapa Bi.Valeria Makonda akizungumza na wanawake wa dawati hilo kabla ya kufanya uchaguzi wa kupata viongozi wa wanawake katika ukumbi wa Gedeco leo 15 Mei, 2023


Na Alphonce  Kabilondo,Geita. 

Mratibu  wa dawati la uwezeshaji wanawake kiuchumi katika halmashauri ya mji Geita Mkoani hapa Valeria  Makonda amesema kuwa majukwa ya wanawake ni sehemu maalum ya wanawake kusemea na kutatua kero zao na kuwaibua wanawake kutoka kwenye wimbi la umasikini.

Mratibu huyo ametoa  kauli hiyo  leo mei 15 mwaka huu  kwenye  uchaguzi wa viongozi wa jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi  ngazi ya halmashauri ya mji uliofanyika kwenye ukumbi wa GEDECO mjini Geita .

Valeria Makonda, Mratibu wa dawati la uwezeshaji wanawake kiuchumi katika halmashauri ya mji Geita  akiratibu zoezi la uchaguzi wa kupata viongozi wapya wa jukwaa la wanawake. 

Makonda amesema  kuwa  lengo la kuanzisha majukwa hayo ni kuwawezesha wanawake kupata sehemu maalumu ya kusemea  changamoto zao na kuzitatua sambamba na kuwawezesha wanawake  kushiriki kikamilifu kwenye shughuli za kiuchumi  hivyo viongozi waliochanguliwa wataliongoza  jukwaa kwa kipindi cha miaka mitatu kwa mujibu wa sheria.

 “Majukwaa haya yapo kwamujibu wa sheria, yameanzishwa kuanzia ngazi ya mitaa vijiji, kata na leo wamefanya  uchaguzi ngazi ya halmashauri ya mji Geita na kuwapata viongozi watakao liongoza jukwaa  kwa kipindi cha miaka mitatu" alisema Makonda .

Valeria Makonda - Mratibu wa dawati la uwezeshaji wanawake kiuchumi katika halmashauri ya mji Geita . 

Awali mwenyekiti wa  uchaguzi huo  Nyakaji Masaluli akitangaza matokeo hayo alitumia fursa hiyo kuwashauri  wanawake hasa viongozi wapya waliochaguliwa kutooneana aibu wakati wa kutekeleza majukumu  kwa kuwachukulia hatua ikiwemo kuwafukuza au kuwaondoa katika nafasi watakaoonekana kuzembea kwa namna yoyote.

Mwenyekiti wa uchaguzi  Bi.Nyakaji Masaluli (wakwanza upande wa kushoto kwako) akiwa tayari kutangaza matokeo ya viongozi wa jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi katika halmashauri ya mji Geita leo 15 Mei, 2023, katikati ni afisa maendeleo ya jamii akifuatilia uchaguzi huo kwa karibu sana na wakwanza kulia ni Saga Mtaki - afisa maendeleo ya jamii na Mratibu wa dawati la maendeleo ya  jinsia. 

Mwenyekiti huyo wa uchaguzi alitangaza matokeo huku akiwataja  viongozi  walio chaguliwa  kwenye uchaguzi huo kwa majina yao na nafasi walizo shinda, ambapo nafasi ya mwenyekiti aliyeshinda na kutangazwa rasmi ni Onester Madata, makamu mwenyekiti Joyce Luchungulila. 

Bi.Nyakaji Masaluli (wakwanza upande wa kushoto kwako) Mwenyekiti wa uchaguzi akitangaza matokeo ya viongozi wapya waliochaguliwa kuongoza jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi katika halmashauri ya mji Geita. 

Aidha wengine waliochaguliwa na kutangazwa rasmi kuwa washindi ni katibu mkuu Jenipha Paschal  huku katibu msaidizi akiwa ni Rachel  Jumbe, mwekahazina ni Conchester Kazaula pamoja na wajumbe watatu wa jukwaa hilo ambao ni Jesca Masota, Halima Masele na Pendo Mawaya. 

Mwenyekiti wa dawati la uwezeshaji wanawake kiuchumi katika halmashauri ya mji Geita ni Onester Madata (kushoto) na  makamu wake ni Joyce Luchungulila (kulia-gauni rangi nyekundu) 

Wajumbe watatu wa jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi katika halmashauri ya mji Geita ni Jesca Masota (mwenye miwani) Halima Masele (anaye andika) na Pendo Mawaya ( aliyeshika mkoba).

Wagombea nafasi ya Katibu wa jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi halmashauri ya mji Geita wakipigiwa kura. 

Wanawake wa jukwaa la uwezeshaji kiuchumi halmashauri ya mji Geita wakifanya uchaguzi wa viongozi wao leo 15 Mei 2023.


Mwisho

Post a Comment

0 Comments