TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

Dkt. JAFARI ASHIRIKI UZINDUZI WA KAMPENI ZA CCM DAR ES SALAAM


Na mwandishi wetu;

Mgombea ubunge wa Jimbo la Busanda kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Jafari Rajabu Seif, amehudhuria uzinduzi wa kampeni za chama hicho uliofanyika leo, Agosti 28, 2025, katika viwanja vya Tanganyika Packers, jijini Dar es Salaam.

Uzinduzi huo umefanyika sambamba na kuanza rasmi kwa kampeni za uchaguzi kwa vyama vyote vya siasa, kwa mujibu wa ratiba ya Tume Huru ya Uchaguzi (INEC).

Tarehe hii inaashiria mwanzo rasmi wa harakati za kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025.

Dkt. Jafari ni miongoni mwa wagombea walioteuliwa na CCM kupeperusha bendera ya chama hicho katika majimbo mbalimbali nchini, yeye akiwakilisha Jimbo la Busanda lililopo Wilaya ya Geita  mkoani Geita.

Uzinduzi huo umeonesha nguvu ya CCM katika maandalizi ya uchaguzi, na umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama, wagombea wa nafasi za udiwani, ubunge, pamoja na wananchi kutoka maeneo mbalimbali.

Post a Comment

0 Comments