TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

DKT. JAFARI AHAHIDI KUSUKUMA AJENDA YA BARABARA KATORO -BUSANDA–NYAKAMWAGA IPITIKE VIPINDI VYOTE

Na mwandishi wetu;

Mgombea ubunge wa Jimbo la Busanda kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Jafari Rajabu Seif, amewahakikishia wananchi wa Kata ya Busanda kuwa atatoa msukumo mkubwa katika ajenda za halmashauri, hasa kwenye uboreshaji wa barabara ya Katoro–Busanda–Nyakamwaga.

 

Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika kata hiyo, Dkt. Jafari amesema kuwa anafahamu changamoto kubwa inayowakabili wananchi kutokana na hali ya barabara hiyo, na kwamba baada ya kuchaguliwa atahakikisha inaboreshwa ili ipitike kipindi chote cha mwaka.

 

 "Nafahamu kuwa barabara yenu ina changamoto. Nitakwenda kusukuma kwa nguvu zaidi ili TANROADS waichukue. Ikishapanda TANROADS, itafanyiwa matengenezo mara mbili kwa mwaka na hivyo itapitika muda wote," amesema Dkt. Jafari.

 Ameongeza kuwa kazi hiyo ni sehemu ya ajenda pana ya kuboresha huduma muhimu kwa wananchi wa Busanda, akiahidi kuendelea kusimamia kwa karibu maendeleo ya kata hiyo na jimbo kwa ujumla.

 

Wananchi wamempongeza mgombea huyo kwa kujitokeza kueleza mipango yake waziwazi, wakisema kuwa barabara hiyo ni kiungo muhimu kwa usafirishaji wa mazao na shughuli za kila siku.

Post a Comment

0 Comments