TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

KIONGOZI MBIO ZA MWENGE AIPONGEZA TARURA, NYANGH'WALE.


Na Editha Edward;


Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Ali Ussi, amesifu mafanikio ya miradi iliyotekezwa na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA), Wilaya ya Nyang'hwale.

 


Hiyo ni mara ya tatu ndani ya siku chache, miradi ya TARURA mkoani Geita kusifiwa na kiongozi wa mbio za Mwenge. Ussi amepongeza ujenzi wa barabara ya Nzera (Geita), barabara ya Kasco (Manispaa ya Geita) na sasa mradi wa ujenzi wa boksi la kalavati katika barabara ya Kharumwa–Nyijundu.

“Niwapongeze sana TARURA, popote nilikopita nikiwa na mwenge huu, nimeona miradi ya kiwango cha juu.  Hata huu mradi, nimeukagua, nimepitia nyaraka zote na hakuna chembe ya shaka.  Huu ni uthibitisho kwamba, fedha za wananchi zinatumika kwa haki, ndiyo maana nauzindua rasmi” ameeleza Ussi




Kwa mujibu wa taarifa iliyosomwa na Meneja wa TARURA Wilaya ya Nyang’wale, Mhandisi John Msita, mradi huo, umegharimu shilingi 579,680,000.00 kupitia ufadhili wa Benki ya Dunia kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

 


Taarifa inaeleza mradi ulikuwa na kazi tatu,  ujenzi wa maboksi ya kalavati mawili ya zege  na matengenezo ya kilometa moja ya barabara ya changarawe. Utekelezaji ulianza Juni 18, 2024 na kukamilika Aprili 14, 2025 chini ya mkandarasi D4N Company Ltd ya Kahama.

 


Aidha, kiongozi wa mbio za mwenge, ametumia fursa hiyo kuwasihi wananchi wa Nyang’wale na Geita,  kujitokeza katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, mwaka huu na wakachague viongozi kwa kuzingatia amani ya nchi



Post a Comment

0 Comments