TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA 2025 AFUNGUA MRADI WA MAJI ULIOTEKELEZWA NA RUWASA


Na Editha Edward;

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Ismail Ali Ussi amelidhishwa na mradi wa kuboresha huduma ya maji katika kijiji cha Inyala na kulishia kuweka jiwe la ufunguzi katika mradi huo ikiwa ni ishara ya kuenzi kauli mbiu ya wizara ya maji ya kumtua mama ndoo kicwani,

 

Akizindua mradi huo kiongonzi wa mbio za mwenge kitaifa mwaka 2025 ameipongeza Ruwasa kwa kukamilisha mradi huo kwa ufasaha huku akiwataka wananchi kuiunga mkono serikali kwa kulinda miundo mbinu ya maji.

Mradi huo wa maji umegharimu zaidi ya milioni mia nne na ulianza kutekelezwa mwaka 2021 na kukamilika mwezi juni 2023 na unatoa huduma ya maji kwa wananchi.

 


Mradi huo umepunguza muda uliokuwa unatumika kufuata maji mbali ambapo sasa muda huo unatumika kufanya shughuli nyingine za uzalishaji na maendeleo kwa jamii. 

Mradi huo umefungua frusa za kiuchumi ikiwemo uendeshaji wa viwanda vidogo vidogo vya kusafisha dhahabu, kufyatua tofari, bustani za miti na mbogamboga na umepunguza magojwa yanayotokana na ukosefu wa maji safi na salama.

 


Post a Comment

0 Comments