TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

KITUO CHA AFYA CHA BILIONI 3 CHAJENGWA MBOGWE, MWENGE WA UHURU WAPONGEZA UWEKEZAJI WA MZAWA.


Na Editha Edward;

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Ismail Ali Ussi amempongeza mwekezaji mzawa aliejenga kituo cha Afya kilichopo kata ya Bukandwe  wilayani mbogwe ili kuwahudumia wakazi wa maeneo hayo.

 

Amesema hayo mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika kituo hicho cha Afya  ambapo amesema kuwa nchi hii inajengwa na watanzania wenyewe na wilaya ya mbogwe inajengwa na wanambogwe wenyewe hivyo wawekezaji wazawa wanao wekeza katika nchi yao wanafanya vyema ili kuwahudumia watanzania wenzao.

 


Ussi amesema kuwa ameisaidia serikali, kwa waliosoma udaktari, fani ya uhudumu, mapokezi kwa wanaoishi mkoa wa Geita  kupata ajira kwani hakuna mwajiliwa mgeni, wote ni wazawa hivyo vijana wetu wamepata kazi katika kituo hicho cha afya. 

 

Akisoma taarifa mkurungenzi wa kituo cha Afya Gakala  Bunga Dadu amesema kuwa mradi huo unathamani ya shiringi bilion tatu.

 


Dadu amesema kuwa  lengo la mradi nikusaidia wananchi wa kata ya Bukadwe  pamoja na kata jirani kupata huduma bora za afya na kibigwa

 


 

Post a Comment

0 Comments