TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

MIRADI YA VISIMA VYA MAJI YAING'ARISHA NYANGH'WALE

Na Editha Edward;

Mwenge wa Uhuru, umeridhishwa na ujenzi wa mradi wa visima vitano vya maji vilivyopo Wilaya ya Nyang'hwale mkoani Geita.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Ismail Ali Ussi, amesema hayo baada ya kukagua mradi huo na kuridhishwa na utekelezaji wake.

 

Amewataka wananchi kushirikiana na viongozi katika kulinda miundombinu ya maji ili iweze kuduma kwa muda mrefu.

Mkuu wa Wilaya ya Nyang'hwale, Grace Kingalame, ametumia fursa hiyo kwa kumshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha katika wilaya hiyo.



Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa RUWASA Mhandisi Suzana Gogadi, amesema vijiji vitano vinanufaika na mradi huo wa maji na kwamba unagharimu zaidi ya milioni miatatu.

 


Mwenge wa Uhuru ukiwa wilaya ya Nyang'hwale utatembelea na kukagua kisha kuweka mawe ya msingi katika miradi 11 yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 1.5

Post a Comment

0 Comments