TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

MNEC EVARIST “CCM INA AHADI ZINAZOTEKELEZEKA, TUKAPIGE KURA KWA WINGI OKTOBA 29”.

Na mwandishi wetu;

 

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa  ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka mkoa wa Geita, Evarist Gervas

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa  ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka mkoa wa Geita, Evarist Gervas, amewataka wananchi wa Kata ya Kamena kukipa kura nyingi CCM katika uchaguzi ujao, akisisitiza kuwa sera na ahadi za chama hicho ni za kweli na zinatekelezwa.

Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika kata hiyo, Gervas amesema kuwa CCM ni chama pekee chenye dira ya maendeleo inayoonekana na inayotekelezwa kwa vitendo kote nchini.

 “Ilani ya CCM inatekelezeka. Vyama vingine havieleweki hata wanatoa ahadi gani. Tuchague chama kinachotekeleza, si cha ahadi zisizoeleweka,” amesema Gervas huku akishangiliwa na wananchi waliohudhuria mkutano huo.

 

Wananchi wa kata ya Kamena waliohudhuria mkutano huo.

Aidha, amewahimiza wakazi wa Kamena kujitokeza kwa wingi kupiga kura siku ya Oktoba 29, ili kuhakikisha kuwa CCM inaendelea kuongoza kwa kishindo na kuleta maendeleo ya kweli kwa wana Kamena.


Post a Comment

0 Comments