TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

GGML WATOA MSAADA WA VIFAA VYA USAFI SOKO LA NYANKUMBU GEITA


Wakwanza kuanzia kushoto wanaozoa taka ni Josephine Kimambo (Mhandisi wa mazingira –GGML) akishiriki katika zoezi la kufanya usafi soko la Nyankumbu Geita, katikati ni Teophil Pima (Afisa mawasiliano-GGML) na kulia ni Mwenyekiti wa soko la Nyankumbu Mchele Mhangwa.

Na  Alphonce  Kabilondo,Geita

Kampuni ya uchimbaji wa madini ya dhahabu Geita Gold  Mine (GGML)  imetoa msaada wa vifaa 8  vya kuhifadhia taka kwa wafanyabiashara wa soko la Nyankumbu  Mtaa wa uwanja  halmashauri ya Mji wa Geita Mkoani hapa .

Mhandisi wa mazingira Mgodi wa GGML  Josephine  Kimambo akitoa elimu ya usafi wa mazingira wakati wa zoezi la kukabidhi vifaa hivyo amesema kuwa  usafi wa mazingira ni muhimu .

Alisema kuwa uchafuzi wa mazngira kwenye soko hilo usipodhibitiwa unaweza kusababisha kuibuka magonjwa ya mulipuko ikiwemo kuhara pamoja na kipindupindu  hivyo jambo la usafi wa mazingira ni mwarobaini pekee .

 Enos Mareli ,Mwenyeki wa mtaa wa uwanja (alievaa gloves kulia) akipokea vifaa vya kuhifadhi taka taka kutoka mgodi wa dhahabu GGML. 

Kimambo alisema kuwa mgodi huo   umekuwa  ukitoa elimu ya uhifadhi wa mazingira kwa jamii kwa makundi tofauti ili kukabiliana na hali ya mabadiriko ya tabianchi . 

“Mgodi wa GGML tutaendelea kutoa elimu ya uhifadhi wa mazingira na kusaidia jamii na kuhakikisha jamii ya geita  inanufaika na uwepo mgodi wa GGML" alisema Kimambo. 

Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa huo Enos Mareli akipokea msaada wa vifaa hivyo ameupongeza uongozi wa mgodi wa GGML  na kuahidi kuwa vifaa hivyo vitatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Aliongeza kuwa vifaa hivyo  vitasaidia kurahisisha ukusanyaji wa taka kwenye masko  mawili ya Mtaa soko la asubuhi  Nyankumbu ,na soko la jioni ambapo ametumia fursa hiyo kuziomba kampuni zingine wadau pamoja na taasisi kuiga mfano wa mgodi huo wa kusaidia jamii .

“Tunaupongeza mgodi wa GGML kwa msaada huu vifaa tulivyo vipokea leo baadhi vitabaki soko la asubuhi nyankubu kifaa kimoja kitapelekwa ofisi ya Mtaa wa Uwanja   lengo ni kudhibiti uchafuzi wa mazingira kwenye masoko hayo" alisema mwenyekiti Mareli .

Vifaa vilivyokabidhiwa na mgodi  wa GGML  kama vinavyoonekana katika picha , nyuma yake ni viongozi wa serikali ya na uongozi wa soko la Nyankumbu mjini Geita na Maafisa kutoka GGML.

Aidha mwenyekiti wa  soko hilo Mchele Mhangwa alisema kuwa vifaa hivyo vimekuja muda mwafaka kabla ya kupata msaada huo walikuwa wakilazimika kufagia taka na kuzibeba kwa kutumia mifuko na kupeleka eneo kukusanyia taka na baadae kusombwa na gari.

Mwisho. 

Post a Comment

0 Comments