TANGAZA NASI: geitapressclub@gmail.com

MBUNGE WA JIMBO LA GEITA MJINI AKABIDHI PIKIPIKI TATU KWA KLABU YA WAANDISHI WA HABARI GEITA

 

Na Samwel Masunzu;



Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Geita (GPC) imesema itaendelea kutimiza wajibu wa kuhabarisha umma na kushiriki huduma za kiuchumi kupitia miradi ya kiuchumi katika jamii

Hayo  yamelezwa na katibu mtendaji msaidizi wa klabu ya waandishi wa habari Mkoa wa Geita Ernest Magashi wakati  wa makabidhiano ya pikipiki tatu ambazo zimenunuliwa kupitia fedha za mfuko wa jimbo la geita

Magashi alisema waliomba kiasi cha shilingi million kumi kutoka Ofisi ya Mbunge wa jimbo la Geita Mjini kupitia mfuko wa jimbo, na amekiri kuwa GPC ilipokea kiasi cha shilingi millioni saba na laki tano, fedha ambayo kamati tendaji ya GPC iliridhia zinunuliwe pikipiki tatu aina ya SanLG zenye thamani ya shilingi milioni sita na laki tisa.

“Tuliomba million kumi kutoka Ofisi ya Mbunge kwaajili ya ununuzi wa pikipiki moja na guta, lakini tulipokea kiasi cha shilingi milioni saba na laki tano ambapo kamati tendaji iliridhia kununua pikipiki tatu badala ya pikipiki moja na guta, na hii ni kutokana na fedha kutokutosheleza kununua pikipiki moja na guta moja kama ilivyokuwa imekusudiwa”Alieleza Magashi




Katibu mkuu msaidizi wa GPC Ernest Magashi(aliyesimama) akielezea kuhusu mradi wa pikipiki ndani ya ofisi za GPC.

Awali kabla ya kukabidhi pikipiki hizo, Mbunge wa jimbo la Geita mjini Costantine Kanyasu amesema hatua hiyo ni kuunga mkono waandishi wa habari kwa kutambua nafasi yao katika jamii.

“Vyombo vya habari ni muhimili wa nne nchini kati ya mihimili mine nchini ambayo ni serikali kuu, mahakama na bunge, hivyo kukosekana kwa waandishi wa habari ni sawa na kukosa jicho”


Mbunge Kanyasu (katikati)akikabidhi funguo za pikipiki kwa Mwenyekiti wa GPC Renatus Masuguliko

Aidha alisema pikipiki hizo zitasaidia kuwafikia wananchi wa vijijini na kuibua kero zao kwa haraka.

Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari mkoni Geita Renatus Masuguliko alishukuru ofisi ya Mbunge kwa kutambua mchango wa vyombo vya habari hasa zilivyopo ndani ya GPC, na kueleza kuwa pikipiki hizo zitasaidia katika kurahisisha shughuli za kiutendaji na kujikwamua kiuchumi na kutokuwa tegemezi.

Hata hivyo baadhi ya wadau wa habari mkoani Geita Ivan Bwoya na Costantine Kalala wamesema katika kuelekea uchaguzi mkuu wanaamini waandishi wa habari ni chachu ya kutoa elimu katika kuwajengea uelewa wananchi.



 Picha ya pamoja: Mbunge, viongozi wa GPC, baadhi ya wanachama na mmoja wa wadau wa habari katika tukio la makabidhiano ya pikipiki februari 20,2025 nje ya ofisi za GPC-Gedeco mjini Geita.

Post a Comment

0 Comments